LIVE STREAM ADS

Header Ads

Kalemani awasweka ndani viongozi wa JUMEME

Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa Binagi Media Group. Mawasiliano 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com

Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani amepiga marufuku makampuni ya kusambaza umeme kwa kutumia nishati mbalimbali ikiwemo jua, kuwatoza wananchi gharama kubwa inayozidi shilingi 100 kwa ankra moja.

Dkt. Kalemani alitoa marufuku hiyo Julai 07, 2020 wakati akizungumza na wananchi katika Wilaya Sengerema mkoani Mwanza, alipokuwa na ziara ya kukagua utekelezaji wa miundombinu mbalimbali  ya kusambaza umeme wilayani humo.

Awali Dkt. Kalemani alipokea malalamiko kutoka kwa wananchi wakiilalamikia kampuni ya JUMEME inayosambaza umeme kwa kutumia nishati ya jua kwa kuwatoza shilingi 3,500 kwa ankra moja ambapo aliamuru viongozi wa kampuni hiyo kukamatwa ili wahojiwe ni kwa nini wanatoza gharama kubwa kinyume na sheria.
Tazama BMG ONLINE TV hapa chini

No comments:

Powered by Blogger.