Wajasiriamali Magu wakabidhiwa mamilioni ya fedha na pikipiki
Akikabidhi
mikopo hiyo Oktoba 23, 2020 Mkuu wa Wilaya Magu, Salum Kali amewataka
walionufaika kuitumia vyema ili kuleta tija katika shughuli zao na kuirejesha
kwa wakati ikizingatiwa kwamba haina riba ili kuwanufaisha wajasiriamali
wengine.
Naye
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Magu, Lutengano Mwalwiba alisema
katika kipindi cha Serikali ya awamu ya tano makusanyo katika halmashauri hiyo yameongezeka
kutoka kiwango cha chini ya bilioni 1.6 hadi kufikia bilioni 3.17 na kuingia
kwenye halmashauri zinazokusanya mapato ya juu ya zaidi bilioni 3.
“Lengo ni
kuongeza zaidi mapato ili kuhakikisha tunatoa huduma bora ikiwa ni pamoja na
mikopo, ni kweli kabisa tumezuia mivujo mingi ya mapato na sasa hali imekuwa
nzuri” aliongeza Mwalwiba.
Na George Binagi-GB Pazzo, BMG
No comments: