LIVE STREAM ADS

Header Ads

Wabunge Wapya Bunge la Afrika Wapewa Semina Elekezi

Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa BMG Online Media. Mawasiliano 0757 43 26 94 ama ripotabmg@gmail.com
Sekretarieti ya Bunge la Afrika (Pan - African Parliament - PAP ) imeendesha semina elekezi kwa Wabunge 11 wapya wa Bunge la Afrika wakiwemo kutoka Burundi, Morocco, Msumbiji, Somalia na Tanzania kabla ya ufunguzi wa Mkutano wa Kwanza wa Kawaida wa Bunge la sita wakati wabunge hao wapya wakitarajiwa kuapishwa.

Semina hiyo imefanyika leo Jumamosi Oktoba 29,2022 katika Makao Makuu ya Bunge la Afrika Midrand Johannesburg Afrika Kusini ambapo wamepewa taarifa muhimu kuhusu kanuni za uendeshaji wa PAP, kazi za Bunge, majukumu yao kama wabunge pamoja na masuala ya fedha, Utawala na Rasilimali Watu.

Wabunge wapya wa Bunge la Afrika kutoka Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni pamoja na Mhe. Anatropia Theonest, Mhe. Toufiq Salim Turkey na Mhe. Ng’wasi Kamani, kutoka nchini Burundi ni Mhe. Bernardine Nduwomana, Morocco ni Mhe. Hannaa Benkhair, Msumbiji ni Mhe. Sarfina Filipe Franco Chindaculema na kutoka Somalia ni Mhe. Seneta Prof. Abdi Ismael Samatar, Mhe. Mohamed Jamal Mursal, Mhe. Abdulrahman Mohamed Hussein, Mhe. Aden Mohamed Nur na Mhe. Zamzam Muhumed Omar.
Kaimu Naibu Karani anayeshughulikia Biashara na Mikutano ya Bunge la Afrika (PAP), Bw. Galal Nassir akizungumza kwenye semina elekezi iliyoandaliwa na Sekretarieti ya Bunge la Afrika (Pan - African Parliament - PAP ) kwa Wabunge wapya wa Bunge la Afrika kwa ajili ya kutoa taarifa muhimu kuhusu kanuni za uendeshaji wa PAP, kazi za Bunge, majukumu yao kama wabunge pamoja na Masuala ya Fedha, Utawala na Rasilimali Watu. 
Picha na Kadama Malunde - Midrand Afrika Kusini
Kaimu Naibu Karani anayeshughulikia Biashara na Mikutano ya Bunge la Afrika (PAP), Bw. Galal Nassir akizungumza kwenye semina elekezi iliyoandaliwa na Sekretarieti ya Bunge la Afrika (Pan - African Parliament - PAP ) kwa Wabunge wapya wa Bunge la Afrika kwa ajili ya kutoa taarifa muhimu kuhusu kanuni za uendeshaji wa PAP, kazi za Bunge, majukumu yao kama wabunge pamoja na Masuala ya Fedha, Utawala na Rasilimali Watu.
Kaimu Naibu Karani Mfawidhi wa Fedha, Utawala na Rasilimali Watu Bunge la Afrika (PAP) Bi. Vivian Abii akizungumza kwenye semina elekezi iliyoandaliwa na Sekretarieti ya Bunge la Afrika (Pan - African Parliament - PAP ) kwa Wabunge wapya wa Bunge la Afrika kwa ajili ya kutoa taarifa muhimu kuhusu kanuni za uendeshaji wa PAP, kazi za Bunge, majukumu yao kama wabunge pamoja na Masuala ya Fedha, Utawala na Rasilimali Watu.
Kaimu Naibu Karani Mfawidhi wa Fedha, Utawala na Rasilimali Watu Bunge la Afrika (PAP, Bi. Vivian Abii akizungumza kwenye semina elekezi iliyoandaliwa na Sekretarieti ya Bunge la Afrika (Pan - African Parliament - PAP ) kwa Wabunge wapya wa Bunge la Afrika kwa ajili ya kutoa taarifa muhimu kuhusu kanuni za uendeshaji wa PAP, kazi za Bunge, majukumu yao kama wabunge pamoja na Masuala ya Fedha, Utawala na Rasilimali Watu.
Wabunge wapya wa Bunge la Afrika kutoka Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Anatropia Theonest na Mhe. Ng’wasi Kamani (kushoto) wakiwa kwenye semina elekezi iliyoandaliwa na Sekretarieti ya Bunge la Afrika (Pan - African Parliament - PAP ) kwa ajili ya kutoa taarifa muhimu kuhusu kanuni za uendeshaji wa PAP, kazi za Bunge, majukumu yao kama wabunge pamoja na masuala ya fedha, Utawala na Rasilimali Watu.
Wabunge wapya wa Bunge la Afrika wakiwa kwenye semina elekezi iliyoandaliwa na Sekretarieti ya Bunge la Afrika (PAP)
Wabunge wapya wa Bunge la Afrika wakiwa kwenye semina elekezi iliyoandaliwa na Sekretarieti ya Bunge la Afrika (PAP)
Wabunge wapya wa Bunge la Afrika wakiwa kwenye semina elekezi iliyoandaliwa na Sekretarieti ya Bunge la Afrika (PAP)
Wabunge wapya wa Bunge la Afrika wakiwa kwenye semina elekezi iliyoandaliwa na Sekretarieti ya Bunge la Afrika (PAP)
Wabunge wapya wa Bunge la Afrika wakiwa kwenye semina elekezi iliyoandaliwa na Sekretarieti ya Bunge la Afrika (PAP)
Wabunge wapya wa Bunge la Afrika wakiwa kwenye semina elekezi iliyoandaliwa na Sekretarieti ya Bunge la Afrika (PAP)
Wabunge wapya wa Bunge la Afrika wakiwa kwenye semina elekezi iliyoandaliwa na Sekretarieti ya Bunge la Afrika (PAP) leo Jumamosi Oktoba 29,2022 katika Makao Makuu ya Bunge la Afrika Midrand Johannesburg Afrika Kusini.
Picha zote na Kadama Malunde - Malunde 1 blog


No comments:

Powered by Blogger.