LIVE STREAM ADS

Header Ads

Kamati ya bunge PAC yaridhishwa mradi wa kiwanda cha mipira ya mikono cha MSD

Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa BMG Media. Mawasiliano 0757 43 26 94 ama ripotabmg@gmail.com

Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya  Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) Japhet Hasunga, akizungumza wakati kamati hiyo ilipotembelea mradi wa kiwanda cha mipira ya mikono cha Bohari ya Dawa (MSD) kilichopo Idofi-Makambako mkoani Njombe. 

Na Mwandishi Wetu, Njombe

KAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) imesema imeridhishwa na maendeleo ya mradi wa kiwanda cha mipira ya mikono cha Bohari ya Dawa (MSD) kilichopo Idofi-Makambako mkoani Njombe na kuahidi kuishauri serikali kuongeza bajeti ya shilingi bilioni 12, kuwezesha mradi huo kukamiloka kuanza kazi ifikapo Julai mwaka huu.

Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya PAC Japhet Hasunga, amesema kamati imeishauri bodi ya Wadhamini MSD na Menejimenti kuwa wabunifu kufikia adhma ya serikali ya Rais Dk.Samia Suluhu Hassan kufikia  uchumi wa viwanda.

Amesema kutokana na tathimini ya Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), inaonyesha ujenzi wa kiwanda hicho umefikia asilimia 70, ambapo kamati imeona haja kwa hatua zilizobaki taasisi za udhibiti kuhakikisha zinashirikiana ipasavyo kuwezesha bidhaa zitakazozalishwa kukidhi viwango vya kimataifa.

Naye Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya MSD, Rosemary Silaa, ameeleza kuwa kiwanda hicho kitakuwa na uwezo wa kuzalisha asilimia 83 ya mahitaji ya mipira ya mikono nchini, ambapo, bodi itahakikisha inaisimamia ipasavyo MSD kufuata kanuni, taratibu na sheria.

Amesema wapo kwenye hatua za kutekeleza mkakati wa kampuni tanzu itakayosimamia shughuli nzima za uzalishaji na MSD kubaki na wajibu wake wa kununua, kutunza na kusambaza bidhaa za afya.

Awali, Mkurugenzi Mkuu wa MSD Mavere Tukai,  aliwasilisha kwa kamati hiyo taarifa ya mradi na kuomba ongezeko la fedha  ili kiwanda kiweze kuanza uzalishaji ipasavyo mwezi Julai mwaka huu na kuwaomba wajumbe hao wa Kamati ya PAC kuwa mabalozi wa mradi huo


 Mkurugenzi Mkuu wa MSD Mavere Tukai,  aliwasilisha kwa kamati hiyo taarifa ya mradi huo.

Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya MSD, Rosemary Silaa, akizungumza wakati wa ziara ya kamati hiyo.
Muonekano wa kiwanda hicho kilichopo Idofi Makambako wilayani Njombe.
Muonekano wa mipira ya mikono inayotengenezwa na kiwandani hicho.
Viongozi wa MSD wakiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa kamati hiyo.
 

No comments:

Powered by Blogger.