LIVE STREAM ADS

Header Ads

MSD YAANDAA SEMINA KWA WAHARIRI VYOMBO VYA HABARI

Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa BMG Media. Mawasiliano 0757 43 26 94 ama ripotabmg@gmail.com
Mkurugenzi Mkuu wa Bohari ya Dawa (MSD), Mavere Tukai
 

Na Dotto Mwaibale, Babati

Bohari ya Dawa (MSD) imeandaa Semina maalum kwa Wahariri wa vyombo vya habari nchini itakayofanyika kwa siku mbili mkoani Dodoma.

Katika taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi Mkuu wa MSD, Mavere Tukai imeeleza kuwa semina hiyo itaanza kesho Aprili 05, 2023 na kufikia tamati kesho kutwa Aprili 06, 2023 na kuwa itafanyika katika ukumbi wa Tume ya Uchaguzi  mkoani humo.

"Lengo la semina hii ni kuwajengea uelewa kuhusu majukumu ya MSD ambayo ni manne ya kuzalisha, kununua, kutunza na kusambaza bidhaa za afya nchini sambamba na maboresho mbalimbali yanayofanywa na taasisi hiyo kupitia mpangomkakati wake wa muda mfupi na mrefu" amesema Tukai.

Tukai amesema mbali na kuwajengea uelewa Wahariri juu ya majukumu na maboresho ya MSD, semina hiyo pia itatoa fursa kwa MSD kutoa ufafanuzi juu ya masuala kadhaa ambayo yamekuwa yakijitokeza kwenye jamii, kufanya ziara naokwenye maghala ya MSD kuangalia mfumo mzima wa mnyororo wa ugavi unavyofanya kazi na kisha kutembelea baadhi ya wateja wa MSD.

No comments:

Powered by Blogger.