LIVE STREAM ADS

Header Ads

Taasisi ya Professor Mwera yawaomba walimu kuanzisha mfuko wa elimu

Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa BMG Media. Mawasiliano 0757 43 26 94 ama ripotabmg@gmail.com
Mkurugenzi wa Taasisi isiyo ya kiserikali ya Professor Mwera Foundation ya mkoani Mara,Hezbon Mwera, akizungumza na wadau wa sekta ya elimu na walimu katika mkutano wa wadau wa elimu 2023 Mkoa wa Singida uliofanyika Aprili 27, 2023.

Na Dotto Mwaibale, Singida

MKURUGENZI  wa Taasisi isiyo ya kiserikali ya Professor Mwera Foundation ya mkoani Mara, Hezbon Mwera amewaomba walimu Mkoa wa Singida kuanzisha mfuko wa elimu ambao utasaidia kwa shughuli mbalimbali katika sekta ya elimu.

Mwera alitoa ombi hilo jana wakati akizungumza na walimu hao kwenye mkutano wa wadau wa elimu mkoa wa Singida  wa mwaka 2023 uliofanyika Aprili 27, 2023, Ukumbi wa Social Mission mjini hapa.

“Nashauri kila halmshauri za mkoa wa Singida kwa kuwashirikisha wadau wengine anzisheni mfuko wa elimu ambao utakuwa ukisaidia kuboresha masualayote yanayohusu elimu katika maeneo hayo na mkoa wa Singida kwa ujumla,” alisema Mwera.

Akizungumzia suala la upatikanaji wa chakula mashuleni alisema jambo hilo linawezekana kwa kuwashirikisha wazazi na kuwa maeneo mengine wameanza kwa kutoa uji na kueleza watoto wanapopata chakula wanafanya vizuri katika masomo yao.

Alisema iwapo wataona wazazi hawatoi ushirikiano katika jambo hilo ni vema siku moja wakaitisha kikao  na wawashindishe njaa kuanzia asubuhi hadi jioni hapo ndipo watakapoona umuhimu wa watoto kupata chakula wakiwa shuleni kwani wapo ambao hawalielewi wakidhani linafanywa na Serikali.

.Aidha, Mwera alisema ili kukabiliana na upungufu wa madarasa na nyumba za walimu aliwaomba  walimu hao kwa kuwashirikisha wadau wengine kuanzisha benki za matofali na kuwa hatua hiyo itakwenda kupunguza changamoto hiyo kwani kuna baadhi ya halmashauri zimefanikiwa kwa kununua mashine za kufyatulia matofali na zimefanya vizuri.

Pia Mwera aliomba walimu kutoka vyuo vya ualimu Mkoa wa Singida wanapo kwenda kufanya mafunzo kwa vitendo ni vizuri wakafanya mafunzo hayo kwenye  shule za mkoani hapa na hata wakati wa likizo wawe wanafanya hivyo na kuwa itaongeza ufaulu kwa wanafunzi kutokana na walimu hao kuwa na moto wa kufundisha..

Halikadharika, Mwera alisema ili kusaidia wanafunzi kufanya vizuri katika masomo yao na kuongeza ufaulu ni kuanzishwa vituo vya vijana kuanzia ngazi ya vitongoji, vijiji,  kata hadi Tarafa ambavyo vitakuwa na mashine zitakazo tumika kudurufu mitihani itakayotumika kwa ajili ya kujifunza vijana hao.

Katika mkutano huo Mwera alipata fursa ya kuelezea shughuli mbalimbali zinazofanywa na taasisi hiyo kuwa ni pamoja na kutoa mafunzo ya ufundi bure  kwa vijana ambapo kwa Wilaya ya Tarime Mkoa wa Mara zaidi ya Sh.Bilioni 3 taasisi hiyo ingezipata iwapo kama ingehitaji kutoa mafunzo hayo kwa kutoza fedha na kuwa vijana 3500 wamenufaika.

Alitaja kazi nyingine ni kuhamasisha vijana wa shule za msingi na sekondari kujiunga na vyuo vya ufundi baada ya kuhitimu, kutoa mafunzo kwa wafanyakazi wa sekta ya hoteli na utalii kwa kuhamasisha utalii wa ndani pamoja na kutoa elimu ya ujasiriamali kwa vijana na wanawake na kuhamasisha watoto wa kike juu ya umuhimu wa shule.

 Pia Mwera alisema taasisi hiyo imekuwa ikisaidia watoto Yatima na wale wanaoishi katika mazingira magumu kupata masomo kuanzia shule ya msingi, Sekondari hadi vyuo vya ufundi. 

Alisema taasisi hiyo awali ilikuwa ikifanya kazi katika mikoa 10 lakini kutokana na kufanya vizuri Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) imetoa kibali kuendelea kufanya kazi katika  mikoa yote ya Tanzania Bara ambapo ameomba maofisa wao watakapokuwa wakipita mikoani  wapewe ushirikiano.

Hivi karibuni taasisi hiyo ya Mkoa wa Mara inayojishughulisha na masuala ya elimu ili mtunuku tuzo ya heshima Rais Dk.. Samia Suluhu Hassan kutokana na mchango wake mkubwa katika maendeleo ya sekta ya elimu nchini, tuzo aliyokabidhiwa  Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule kwa niaba yake.

Mkuu wa Mkoa wa Singida, Peter Serukamba (kushoto) akimkabidhi cheti Mkurugenzi wa Taasisi isiyo ya kiserikali ya Professor Mwera Foundation ya mkoani Mara, Hezbon Mwera baada ya taasisi hiyo kutoa baadhi ya tuzo za heshima kwa washindi.
Mkurugenzi wa Taasisi isiyo ya kiserikali ya Professor Mwera Foundation ya mkoani Mara,Hezbon Mwera (kulia) akiwa meza kuu na viongozi waliohudhuria mkutano huo. Kutoka kushoto ni Afisa Elimu Mkoa wa Singida, Dk.Baganda Elpidius, Mkuu wa Wilaya ya Singida, Mhandisi Paskas Muragili, Katibu Tawala Tawala, Mkoa wa Singida, Dk.Fatma Mganga, Mkuu wa Mkoa wa Singida, Peter Serukamba, Katibu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Singida, Lucy Boniface na Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Singida, Lucia Mwiru.
Mkurugenzi wa Taasisi isiyo ya kiserikali ya Professor Mwera Foundation ya mkoani Mara,Hezbon Mwera, akiwa na Afisa Elimu Mkoa wa Singida, Dk.Baganda Elpidius baada ya kumalizika kwa mkutano huo.
Mkurugenzi wa Taasisi isiyo ya kiserikali ya Professor Mwera Foundation ya mkoani Mara, Hezbon Mwera (kulia) akiwa kwenye mkutano huo.

Wadau wa sekta ya elimu na walimu wakiwa kwenye mkutano huo.
Taswira ya makutano huo.

No comments:

Powered by Blogger.