LIVE STREAM ADS

Header Ads

Mwenge wa Uhuru 2023 watua Mkalama, Singida

Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa BMG Media. Mawasiliano +255 757 432 694 ama ripotabmg@gmail.com
Mkuu wa Wilaya ya Mkalama, Moses Machali (kulia) akikabidhiwa Mwenge wa Uhuru 2023 na Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Suleiman Mwenda baada ya kumaliza mbio zake wilayani humo Septemba 23, 20223 katika makabidhiano yaliyofanyika Viwanja vya Chuo cha Ufundi cha FDC kilichopo Kata ya Msingi wilayani humo.

Na Dotto Mwaibale, Mkalama
Wilaya ya Mkalama mkoani Singida imepokea Mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2023 kutoka Wilaya ya Iramba mapokezi yaliyofanyika Septemba 23, 2023 Kata ya Msingi wilayani humo na kupongezwa kwa utekelezaji wa miradi ambapo kesho alfajiri Septemba 24, 2023 utakabidhi mbio hizo Wilaya ya Singida DC.

Akizungumza wakati akiupokea Mwenge wa Uhuru, Mkuu wa Wilaya ya Mkalama, Moses Machali amesema ukiwa wilayani humo utatembelea, utakukagua, kufungua, kuzindua na kuweka jiwe la msingi kwenye miradi mbalimbali yenye thamani ya Sh. Bilioni 1.7.

"Mwenge wa Uhuru ukiwa katika wilaya yetu utakimbia umbali wa kilometa 150.8 na kupitia miradi ya elimu, afya, maji,barabara, programu za vijana, utunzaji wa mazingira, masuala ya ujasiriamali na mambo mengine" amesema Machali.

Amesema ukiwa katika wilaya hiyo Mwenge huo utakimbizwa katika tarafa tatu na kwenye kata mbalimbali ambapo wananchi watapata fursa ya kuushangilia na kuwaweka pamoja na kupitia kauli mbiu ya Mwenge wa Uhuru ya mwaka huu isemayo Tunza Mazingira, Okoa Vyanzo vya maji kwa Ustawi wa Viumbe Hai na Uchumi wa Taifa watazindua programu ya utunzaji wa mazingira kwa kupanda miti zaidi ya 500 katika Shule ya Msingi Mayelu.

"Niwakaribisheni wakimbiza Mwenge wa Uhuru Kitaifa katika wilaya yetu ya Mkalama tumejiandaa vizuri na tutashirikiana kuukimbiza katika maeneo yote na nichukue nafasi hii kuwapongeza wananchi kwa kujitokeza kwa wingi kupokea Mbio za Mwenge wa Uhuru kwa mwaka huu 2023” amesema Machali.

Akizungumza na wananchi kwa nyakati tofauti wakati akitembelea miradi hiyo kiongozi wa mbio hizo, Abdalla Shaib Kaim amesisitiza kuwepo na uaminifu, uzalendo na usimamizi wa kina kwenye miradi ya maendeleo kwa kuzingatia kuwa fedha nyingi zimetolewa na Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan hivyo ni vizuri miradi hiyo ikakamilika kwa thamani halisi na si vinginevyo.

Mkimbiza mwenge huyo ameipongeza Wilaya hiyo kwa kukamilisha miradi kwa kiwango cha juu na akaomba zile kasoro ndogondogo zilizojitokeza katika baadhi ya miradi kuzirekebisha.

Aidha Kaim akishiriki kupanda miti katika Shule ya Msingi Mayelu amehimiza suala zima la utunzaji wa mazingira katika maeneo mbalimbali ya wilaya hiyo.

Akitoa neno la shukrani Mbunge wa Jimbo la Iramba Mashariki, Francis Isack amemshukuru Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuijali Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama kwa kutoa fedha nyingi kwa ajili ya miradi mbalimbali na akawaomba wananchi kumpa zawadi ya kipekee kwa kumpa kura nyingi wakati wa uchaguzi mkuu utakaofanyika mwaka 2025.

Baadhi ya miradi iliyotembelewa na Mwenge wa Uhuru Mwaka 2023 ni Matengenezo ya barabara za Mwando-Mng'anda- Mwanga (Km 12.39) na Ishenga- Iambi (Km 4.12) mradi ambao upo Tarafa ya Nduguti, Kata ya Nduguti na Ilunda ambao umegharimu Sh.314,986,600.82 fedha zilizotolewa na Serikali kuu kupitia tozo.

Miradi mingine ni wa vijana wa kilimo cha nyanya, ujenzi wa miundombinu ya mradi wa maji katika Kijiji cha Malaja ambao umegharimu Sh.565,000,000 ambao utawapunguzia adha wananchi wapatao 6,611 kwa kufuata maji umbali mrefu, Programu ya mapambano dhidi ya malaria ambapo wilaya hiyo imeweza kutoa vyandarua 22,098 kwa walengwa ambao ni wajawazito 8,116 na watoto chini ya umri wa mwaka mmoja 9,782.

Miradi mingine iliyotembelewa ni ujenzi wa Shule ya Msingi Nkindiko, uzinduzi wa daraja la Iambi na uzinduzi wa Klabu ya kupinga rushwa katika Shule ya Nduguti Pre And Primary English Medium School.
Vijana wa Skauti, Wansinguya Edward (kushoto) na Elia Kamata wakifanya itifaki kwa kumvika Skafu Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru 2023, Abdalla Shaib Kaim kabla ya kuanza mbio za mwenge huo wilayani Mkalama.
Vijana wa Skauti, wakifanya itifaki kwa kumvika Skafu Mkimbiza Mwenge wa Uhuru 2023, Tupokigwe Elia kabla ya kuanza mbio za mwenge huo wilayani Mkalama.
Mkuu wa Polisi Wilaya ya Mkalama (SSP) Richard Mwaisemba, akiwa ameushika Mwenge wa Uhuru kabla ya kuanza kukimbizwa wilayani humo.
Watoto wakionesha furaha zao wakati wa kuupokea mwenge huo.
Hamasa zikifanyika wakati wa mapokezi ya mwenge huo.
Wakimbiza Mwenge wa Uhuru Wilaya ya Mkalama wakiwa tayari kwa kukimbiza mwenge huo. Kutoka kushoto ni Emilian Masheyo, Iddi Juma, Abdul Said, Plasido William, Karoline Remiji na Maria Sekidava.
Wanafunzi wa Chuo cha Ufundi cha FDC Wilaya ya Mkalama wakiwa kwenye mapokezi hayo.
Vijana wa Skauti wakiwatayari kwa mapokezi ya Mwenge wa Uhuru.
Viongozi, wakuu wa idara na wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama wa wilaya hiyo wakiwa kwenye mapokezi ya mwenge huo.
Vijana wa Halaiki wakiwajibika wakati wa mapokezi ya Mwenge wa Uhuru 2023..
Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Suleiman Mwenda (wa pili kulia) akiongoza kukimbiza Mwenge wa Uhuru 2023 kabla ya kuukabidhi kwa Wilaya ya Mkalama.,
Mwenge wa Uhuru 2023 ukikimbizwa baada ya kuwasili wilayani Mkalama.
Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru 2023, Abdalla Shaib Kaim akizungumza na viongozi wa Wilaya ya Iramba wakati alipokuwa akiwaaga kabla ya kuanza kuukimbiza mwenge huo wilayani Mkalama.
Muonekano wa shamba la nyanya la vijana wa Mkalama ambalo lilikaguliwa na viongozi wa mbio za mwenge.
Nyaraka za mradi wa shamba la nyanya la vijana hao zikikaguliwa na viongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru 2023.
Mwonekano wa shamba darasa la Programu ya Lishe lililopo Shule ya Msingi Mayelu.
Wanafunzi wa Shule ya Msingi Mayelu wakiwa katika mapokezi ya Mwenge wa Uhuru wakati ulipofika kukagua miradi mitatu inayotekelezwa shuleni hapo ambayo ni programu ya lishe, Utunzaji mazingira na ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa.
Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru 2023, Abdalla Shaib Kaim, akivuta pazia kuashiria uwekaji wa jiwe la msingi la ujenzi wa darasa katika shule hiyo. Kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Mkalama, Moses Machali.
Muonekano wa moja ya darasa lililojengwa katika shule hiyo.
Ukaguzi na uwekaji wa jiwe la mradi wa maji wa Kijiji cha Malaja ukifanyika.
Wananchi wakiwa katika hafla ya uwekaji wa jiwe la msingi wa ujenzi wa barabara za Mwando-Mng'anda- Mwanga (Km 12.39) na Ishenga- Iambi (Km 4.12).
Ukaguzi wa daraja la Iambi ukifanyika.
Wananchi wa Kijiji cha Iambi wakiserebuka wakati wa uwekaji wa jiwe la msingi wa ujenzi wa barabara hiyo.
Muonekano wa jengo la Utawala la Shule ya Msingi, Nkindiko iliyokaguliwa na mbio za Mwenge wa Uhuru 2023. iliyopo Kata ya Ishenga wilayani humo.
Wananchi wa Kata ya Ishenga wakiwa kwenye hafla ya kuupokea Mwenge wa Uhuru baada ya kuwasili kutembelea na kuikagua shule hiyo.
Muonekano wa baadhi ya madarasa ya shule hiyo.
Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru 2023, Abdalla Shaib Kaim, akigawa vyandarua kwa wajawazito kupitia mradi wa kupambana na malaria kwa wajawazito na watoto walio na umri chini ya mwaka mmoja unaoendeshwa na Hospitali ya Wilaya ya Mkalama.
Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru 2023, Abdalla Shaib Kaim, akishirikiana na Mkuu wa Wilaya ya Mkalama, Moses Machali wakiteketeza pombe haramu aina ya Gongo ambayo ilikamatwa na jeshi la polisi wilayani humo. Anayeshuhudia kulia ni Mkuu wa Polisi Wilaya ya Mkalama, SSP Richard Mwaisemba.
Wanafunzi wa Shule ya Nduguti Pre And Primary English Medium School wakiimba nyimbo baada ya Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru 2023, Abdalla Shaib Kaim, kuzindua Klabu ya Kupinga vitendo vya rushwa.
Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru 2023, Abdalla Shaib Kaim, akikabidhiwa taarifa ya uanzishwaji wa klabu hiyo ya kupinga rushwa iliyoanzishwa katika shule hiyo.
Askari wa Jeshi la Akiba wakihimarisha ulizi katika mkutano baada ya Mwenge wa Uhuru 2023 kuwasili eneo ambalo utakesha.

No comments:

Powered by Blogger.