LIVE STREAM ADS

Header Ads

Mahafali ya kwanza Hope Extended Excellence yafana

Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa BMG Media. Mawasiliano +255 757 432 694 ama ripotabmg@gmail.com
Jumla ya wanafunzi 23 wamehitimu elimu sekondari mwaka 2023 kwa mara ya kwanza katika shule ya Hope Extended Excellence Secondary School iliyopo katika Manispaa ya Shinyanga Mkoani Shinyanga.

Akizungumza wakati mahafali ya kwanza katika shule ya Sekondari Hope Extended Excellence Afisa Elimu Sekondari Manispaa ya Shinyanga Lucas Mzungu kwa niaba ya Mkurugenzi wa Manispaa ya Shinyanga amewahimiza wazazi na walezi kufuatilia maendeleleo ya watoto shuleni.

Aidha amewataka wazazi na walezi kuwekeza kwenye elimu ya watoto wao kama ambavyo serikali imekuwa ikifanya kupitia mfumo wa elimu bure.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa shule za Hope Extended Excellence zilizopo Manispaa ya Shinyanga, Bahati Bulongo Dede amesema Ushirikiano unaotolewa na serikali ikiwa ni pamoja na uratibu na ushauri kwa wawekezaji katika sekta binafsi pamoja na uwepo wa mazingira mazuri ya uwekezaji imekuwa ni chachu ya kuvutia uwekezaji katika sekta ya elimu nchini.
Afisa Elimu Sekondari Manispaa ya Shinyanga Lucas Mzungu akizungumza wakati wa Mahafali ya kwanza katika shule ya Hope Extended Excellence Secondary School iliyopo katika Manispaa ya Shinyanga Mkoani Shinyanga.
Afisa Elimu Sekondari Manispaa ya Shinyanga, Lucas Mzungu akizungumza wakati wa Mahafali ya kwanza katika shule ya Hope Extended Excellence Secondary School iliyopo katika Manispaa ya Shinyanga Mkoani Shinyanga.
Mkurugenzi wa shule za Hope Extended Exellence zilizopo Manispaa ya Shinyanga, Bahati Bulongo Dede akizungumza wakati wa Mahafali ya kwanza katika shule ya Hope Extended Excellence Secondary School iliyopo katika Manispaa ya Shinyanga Mkoani Shinyanga.
Wahitimu wakisoma risala wakati wa Mahafali ya kwanza katika shule ya Hope Extended Excellence Secondary School iliyopo katika Manispaa ya Shinyanga Mkoani Shinyanga.
Zoezi la kukata keki likiendelea wakati wa Mahafali ya kwanza katika shule ya Hope Extended Excellence Secondary School iliyopo katika Manispaa ya Shinyanga Mkoani Shinyanga.
Wahitimu wakiwa kwenye Mahafali ya kwanza katika shule ya Hope Extended Excellence Secondary School.
Wahitimu wakiwa kwenye Mahafali ya kwanza katika shule ya Hope Extended Excellence Secondary School.
Wahitimu wakiwa kwenye Mahafali ya kwanza katika shule ya Hope Extended Excellence Secondary School.
Wahitimu wakitoa burudani kwenye Mahafali ya kwanza katika shule ya Hope Extended Exellence Secondary School.
Wahitimu wakitoa burudani kwenye Mahafali ya kwanza katika shule ya Hope Extended Excellence Secondary School.
Wahitimu wakitoa burudani kwenye Mahafali ya kwanza katika shule ya Hope Extended Excellence Secondary School.

No comments:

Powered by Blogger.