LIVE STREAM ADS

Header Ads

Wajasiriamali watakiwa kuongeza thamani ya bidhaa zao

Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa BMG Media. Mawasiliano +255 757 432 694 ama ripotabmg@gmail.com
Afisa Tarafa ya Ilongero Wilaya ya Singida, Yahaya Njiku, akizungumza wakati akifungua mafunzo ya wajasiriamali.


Na Dotto Mwaibale, Singida
Afisa Tarafa ya Ilongero Wilaya ya Singida, Yahaya Njiku amewahimiza wajasiriamali katika tarafa hiyo kuongeza thamani ya bidhaa wazazozizalisha ili ziuzwe kwa bei ya juu jambo litakalo saidia kuinuka kiuchumi.

Njiku ametoa ombi hilo wakati akifungua mafunzo ya ujasiriamali kwa wananchi wa tarafa hiyo ambayo yaliandaliwa na Shirika lisilo lakiserikali Star Entrepreneur General lenye makao yake makuu mkoani Singida.

Amesema mafunzo hayo ni ya muhimu kwa wananchi wa tarafa hiyo kwani yamelenga kuwainua wananchi kiuchumi kuanzia ngazi ya familia hadi taifa.

“Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Dkt. Samia Saluhu Hassani imejielekeza kuwawezesha wajasirimali na wafanya biashara wadogo ili kukuza mnyororo wa thamani wa bidhaa wanazozalisha hivyo ni vizuri mkatumia mazingira na rasilimali zinazowazunguka kwa kuzigeuza kuwa fursa katika uwekezaji” amesema Njiku.

Njiku amepongeza shirika hilo kwa kuunga mkono jitihada za Serikali kwa kutoa mafunzo hayo kwa wajasiriamali hao na akaomba mashirika mengine yaliyoyopo katika wilaya hiyo kuiga mafano wa shirika hilo.

Amesema kupitia mafunzo hayo wananchi wanajiajiri kupitia utengenezaji wa bidhaa zao ambazo wanaziuza ndani ya Mkoa wa Singida na mikoa jirani.

Naye Mkurugenzi wa Shirika la Star Entrepreneur General, Danford Kassaga amesema mafunzo hayo yatawawezesha wafanyabiashara na wajasiriamali hao kujifunza mbinu za kibiashara na kujua namna ya kukuza thamani ya bidhaa zao.

Washiriki wa mafunzo hayo wamenufaika kwa kujifunza utengenezaji wa vitu mbalimbali kama sabuni, uokaji wa keki kwa ajili ya sherehe, upikaji wa tambi za mayai, unga wa lishe, ufugaji wa kuku,utengenezaji wa batiki pamoja na usimamizi wa biashara na masoko.
Mkurugenzi wa Shirika la Star Entrepreneur General, Danford Kassaga akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo.
Afisa Tarafa ya Ilongero Wilaya ya Singida, Yahaya Njiku akisisitiza jambo wakati akifungua mafunzo hayo.

No comments:

Powered by Blogger.