LIVE STREAM ADS

Header Ads

Kapinga awataka wananchi kutunza miuondombinu ya umeme

Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa BMG Media. Mawasiliano +255 757 432 694 ama ripotabmg@gmail.com
Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Judith Kapinga amewataka wananchi kuhakikisha wanalinda na kutunza miundombinu ya umeme nchini ili itumike kwa muda mrefu.

Amesema hayo Novemba 29, 2023 mkoani Morogoro wakati akiwasha umeme kwa mara ya kwanza katika vijiji vya Maseyu na Newland vilivyopo katika Kata ya Gwata katika ziara yake ya kukagua utejekezaji wa miradi ya Wakala wa Nishati Vijijini (REA) mkoani humo.

Amesema serikali imekuwa ikitumia fedha nyingi katika utekelezaji wa miradi ya kusambaza umeme vijijini lengo likiwa ni kuharakisha maendelea, hivyo wanapaswa kusaidia kulinda miundimbinu hiyo ili iwanufaishe wananchi wengi na kwa muda mrefu.

“Msiruhusu upenyo wa mtu kuhujumu miundombinu, tuhakikishe tunailinda kwani serikali imewekeza fedha nyingi na tuipe thamani inayostahili” amesema Naibu Waziri Kapinga wakati akizungumza na wananchi wa vijiji vya Maseyu na Newland mkoani Morogoro.
Amesema serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imejipambanua kwa kuwaletea wananchi maendeleo kwa kuweka miundombinu wezweshi ili waweze kushiriki shughuli mbali mbali za uchumi.

Serikali ya Awamu wa Sita ni ya maendeleo hivyo wananchi wanapaswa kutumia huduma ya upatikanaji wa umeme vijijini kujiinua kiuchumi kwa kuutimia katika shughulli za biashara.

Naibu Waziri Kapinga amewataka wakandarasi wanaojenga miradi ya REA kuhakikisha wanaikamilisha kwa wakati ili ifikapo Juni 2024 miradi yote iwe imekamilika.
Akielezea utekelezaji wa miradi, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa REA, Mhandisi Jones Olotu amesema serikali imewekeza jumla ya shillingi 114.6 billioni kwa miradi mitano inayotekelezwa kwa Mkoa wa Morogoro.

Amesema Serikali kupitia REA inaendelea kutekeleza miradi mbalimbali nchi nzima pamoja na kuwasimamia kwa karibu wakandarasi wote waliopewa zabuni yakutekeleza miradi mbalimbali ya umeme ili kuhakikisha miradi hiyo inakamilika kwa wakati na kwa ubora uliopangwa.

Mhandisi Olotu amesema mkoa wa Morogoro una jumla ya vijiji 669 ambapo hadi kufikia sasa vijiji 583 sawa na asilimia 87.1% vimepata huduma ya umeme kupitia mitano.

Ameitaja miradi hiyo kuwa ni REA Awamu ya Tatu Mzunguko wa Pili (REA III Round II), Mradi wa Kituo cha Kupoozea Umeme cha Ifakara, Mradi wa ujazilizi (Densification IIB), Mradi wa Kupeleka umeme kwenye migodi midogo na maeneo ya kilimo na Mradi wa Kupeleka umeme kwenye Vituo vya Afya na Pampu za Maji.

Kwa upande wake, Mbunge wa Morogoro Kusini Mashariki, Mhe. Khamis Taletale aliishukuru serikali kwa utekelezaji wa kwa kutoa fedha za kutosha kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya nishati vijini jimboni kwake.
Imeandaliwa na Issa Sabuni, Zuwena Msuya, Morogoro

No comments:

Powered by Blogger.