LIVE STREAM ADS

Header Ads

TBS YATOA ELIMU KWA WAJASIRIAMALI KUHUSU ALAMA YA UBORA

Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa BMG Media. Mawasiliano +255 757 432 694 ama ripotabmg@gmail.com
Shirika la Viwango Tanzania (TBS) limeendelea kutoa Elimu kwa wajasiriamali na wazalishaji wa bidhaa Katika Jukwaa la Uwezeshaji wanawake kiuchumi lilofanyika katika ukumbi wa JINCC Jijini Dar es Salaam kwa lengo la kuwasaidia kutambua namna ambavyo wataweza kupata alama ya ubora ya TBS kwenye bidhaa zao ili kuziongezea thamani.

Akizungumza na waandishi wahabari Dec 19,2023 katika ukumbi wa JNICC Dar es Salaam Afisa Udhibiti Ubora, Bw.Christopher Magafu amesema watu wengi wamekuwa hawana uwelewa jinsi ya kupata alama ya ubora ya TBS hivyo wamehudhuria mahali hapo ili kutoa Elimu namna watakavyoweza kufanya mchakato wa kupata alama hiyo ya ubora ya TBS.

"Tunaamini kupitia elimu hii itaweza kurahisisha mawazo yao madogo kuyafanya yawe makubwa,kimsingi wajasiriamali hadi Sasa hivi serikali yetu imeweza kuwarahisishia sana kila mwaka serikali imekuwa ikitenga fungu maalumu kwa ajili ya kuwasaidia wajasiriamali wadogo na wa kati ili tu waweze kupata alama ya ubora". Amesema Bw. Magafu.

Aidha amebainisha kuwa ili kupata msamaha Kuna viambatanisho vya utambulisho kutoka SIDO ambapo kupitia utambulisho huo utaweza kumpatia nafasi mjasiriamali kupata nafasi ya kufanya maombi ya kupata alama hiyo ya ubora.

"Wakija kwetu kupitia utambulisho wa SIDO sisi tutaweza kuwatambua na kuanza kufanya maombia kwenye mfumo wetu wa TBS ambapo akiingia katika mfumo wa www.tbs.go.tz ataona kitufe Cha E-Service ambapo atakutana na option ya i-SQMT Portal ambapo wajasiriamali wote na wafanyabiashara wote wapo hapo". Ameeleza.

Amesema lengo la TBS ni kuhakikisha wajasiriamali na wazalishaji wa bidhaa wanazalisha bidhaa ambazo zimepitia Viwango stahiki na kulinda usalama wa mlaji.
Na Emmanuel Mbatilo, Dar

No comments:

Powered by Blogger.