LIVE STREAM ADS

Header Ads

Mradi wa kuzuia kuzama maji Ziwa Victoria watambulishwa Mwanza

Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa BMG Media. Mawasiliano +255 757 432 694 ama ripotabmg@gmail.com
Shirika la mazingira na maendeleo EMEDO limeutambulisha mradi wa kuzuia watu kuzama maji katika Ziwa Victoria kwa wadau mbalimbali wa uvuvi mkoani Mwanza.

Afisa Mradi huo, Arthur Mgema amesema lengo ni kuzuia vifo vitokanavyo watu kuzama maji katika Ziwa Victoria hasa wavuvi, watoto na wanawake wachakataji wa mazao ya samaki/ dagaa ambao wako kwenye hatari zaidi.

Akifungua kikao cha kuutambulisha mradi huo, Katibu Tawala Mkoa Mwanza, Elikana Balandya amesema matukio ya watu kuzama maji yanazuilika endapo kila mmoja atatimiza wajibu wake.

Amesema kwa Mkoa Mwanza Serikali inatekelezeka mpango wa BBT (Building Better Tomorrow) katika sekta ya ufugaji na uvuvi hivyo mradi wa kuzuia kuzama maji katika Ziwa Victoria utasaidia kutoa elimu ili kuzuia vifo zitokanavyo na kuzama maji.

Mradi wa kuzuia kuzama maji katika Ziwa Victoria unatekelezwa na shirika la EMEDO katika mikoa ya Mwanza, Mara na Kagera katika kipindi cha miaka mitatu hadi mwaka 2025 kwa ufadhili wa taasisi ya RLNI- Life Boats ya nchini Uingereza.
Na George Binagi- GB Pazzo, BMG
Afisa Mradi wa kuzuia kuzama maji Ziwa Victoria, Arthur Mgema (kulia) akimkabidhi Katibu Tawala Mkoa Mwanza, Elikana Balandya (kushoto) ripoti ya utafiti uliofanywa na shirika la EMEDO mwaka 2021 kuhusu sababu za wavuvi kuzama maji pamoja na rasimu ya uvuvi salama iliyoandaliwa katika mwalo wa Busekera mkoani Mara.
Katibu Tawala Mkoa Mwanza, Elikana Balandya akifungua kikao cha kuutambulisha mradi wa kuzuia kuzama maji katika Ziwa Victoria kilichowakutanisha wadau jijini Mwanza.
Afisa Mradi wa kuzuia kuzama maji Ziwa Victoria, Arthur Mgema akieleza kuhusu mradi huo ambao umelenga kutoa elimu kwa jamii ya wavuvi ili kuchukua tahadhari za kuzuia kuzama maji.
Kaimu Afisa Maendeleo Mkoa Mwanza, Rehema Mkinze akizungumza wakati wa ufunguzi wa kikao cha kuutambulisha mradi wa kuzuia kuzama maji Ziwa Victoria.
Wadau mbalimbali mkoani Mwanza wakifuatilia kikao cha kuutambulisha mradi wa kuzuia kuzama maji katika Ziwa Victoria.
Kwa mujibu wa shirika la afya duniani (WHO) watu 236,000 hupoteza maisha kwa kuzama maji. Hata hivyo bado kuna changamoto ya upatikanaji wa takwimu za watu wanaofariki kwa kuzama maji katika mataifa mbalimbali duniani, Tanzania ikiwemo hivyo pamoja na mambo mengine, pia mradi wa kuzuia kuzama maji Ziwa Victoria utasaidia upatikanaji wa takwimu hizo.
SOMA PIA>>> HABARI ZAIDI HAPA

No comments:

Powered by Blogger.