Rais Samia ampongeza Rais Mteule Namibia
Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa BMG Media. Mawasiliano +255 757 432 694 ama ripotabmg@gmail.com
Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ametuma salamu za pongezi kwa Rais mteule wa Namibia, Netumbo Nandi-Ndaitwah.
"Kwa niaba ya Serikali na Wananchi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, natoa pongezi zangu za dhati kwa Mheshimiwa Netumbo Nandi-Ndaitwah, Rais Mteule wa Jamhuri ya Namibia, kwa ushindi wako wa kihistoria katika uchaguzi mkuu wa 2024 nchini Namibia.
"Ninatarajia kufanya kazi nawe katika kuimarisha uhusiano wa kindugu na uhusiano wa kihistoria kati ya Tanzania na Namibia".
#KAZIINAONGEA
No comments: