LIVE STREAM ADS

Header Ads

Nishati ya uhakika inakuza uchumi- Biteko

Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa BMG Media. Mawasiliano +255 757 432 694 ama ripotabmg@gmail.com
Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dkt. Doto Biteko amesema kuwa ukuaji wa uchumi wa nchi yoyote unategemea upatikanaji wa nishati ya uhakika na yenye gharama nafuu.

"Kwa nchi yoyote inayotaka kukua kwa kiasi kikubwa inategemea Nishati inayopatikana kwa hakika na yenye bei nafuu, Bila nishati ya gharama nafuu, uchumi utabadilika na bidhaa zitazalishwa kwa gharama kubwa zaidi" amesema Dkt. Biteko.

Dkt. Biteko ameyasema hayo Januari 10,2025 akihijiwa na TBC na kusisitiza kuwa Serikali ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imejipanga kuhakikisha umeme wa uhakika unapatikana kwa gharama nafuu ili kuchochea maendeleo ya kiuchumi na kuboresha maisha ya wananchi.

No comments:

Powered by Blogger.