LIVE STREAM ADS

Header Ads

SEHEMU YA NNE: TARIME ZIPO MILA ZA KUKUMBATIA, LAKINI SI UKEKETAJI.


Wasichana wakikeketwa
Jambo la kusikitisha ni kwamba idadi hiyo bado ni kubwa sana na inatishia mbaya zaidi hiyo ni idadi ya koo moja ya kabila la Wakurya, ambapo itakumbukwa kuwa kabila la wakurya linaundwa na jumla ya koo 13 na zote zinatekeleza mila hiyo japo kila moja katika kipindi tofauti.
 
Ukweli ni kwamba elimu zaidi inahitajika kutolewa kwa wazee wa kimila, mangariba sanjari na jamii nzima kwa ushirikiano wa karibu kabisa na serikali pamoja na wadau mbalimbali yakiwemo mashirika na taasisi binafsi ili kuweza kuwaokoa wasichana hawa kutoka katika janga hili la ukeketaji.

Jukumu la kupambana na vitendo vya ukeketaji ni la jamii nzima, ambapo hapo kuna kundi kubwa la waalimu ambalo lina nafasi mhimu katika kutoa elimu wa watoto wa kike juu ya kupinga suala hili kama ilivyopendekezwa na Mwalimu Irene Massau kutoka shule ya msingi Kibumaye alipokuwa akizungumza na mwandishi wa makala hii.

“Tunaomba serikali iweze kutumia asasi za watu binafsi ili waweze kutoa elimu kwa walimu; ili walimu nao waanze kutoa elimu kwa wanafunzi ili waweze kujua madhara ya ukeketaji; kwa sababu wakishakeketwa huwa wengi wao unakuta wanapata mimba za utotoni; unakuta mototo ana  miaka 15 anaolewa na matokeo yake anapata mimba ambapo matokeo ya mimba za utotoni yanasababisha vifo” alisema mwalimu Massau.

Mpenzi msomaji matarajio yangu ni kwamba utakuwa wa kwanza kuchukua hatua ya kuokoa japo kwa kutoa taarifa katika vyombo vya dola ama taasisi zilizo mstari wa mbele katika kupigania haki za watoto wa kike katika kutokomeza kitendo hiki katili cha ukeketaji.

Lakini kabla sijahitimisha labda nikueleze tu kwamba katika makala hii nimeamua kujikita tu katika Mila ya ukeketaji ambayo imekuwa mwiba mkali kwa watoto wa kike katika Wilaya ya Tarime, lakini kama ulikuwa na kiu ya kuzifahamu baadhi ya mila na desturi ambazo ni mhimu kuenziwa katika Wilaya hiyo basi ni pamoja na Mila ya Kuzindika.

Mila hii hutekelezwa katika kipindi maalumu kama vile kipindi cha njaa ama vita ambapo mnyama huchinjwa na watu hula sanjari na kunywa pombe ya asili kama vile machicha  kwa lengo la kuondoa majanga (nuksi) kama hayo (njaa ama vita nk) katika jamii.

MTANZANIA MEDIA: Kusoma Makala hii kuanzia mwanzo hadi Mwisho bonyeza MAKALA utasoma kuanzia seheme ya kwanza hadi ya nne. Maoni na Ushauri 0757 43 26 94.

No comments:

Powered by Blogger.