LIVE STREAM ADS

Header Ads

KOMBE LA DUNIA: OIRIGI NI NOMA, AISAIDIA UBELJIJI KUSONGA MBELE.

Divock Origi aifungia Ubeljiji bao la Ushindi.

Tineja aliyezaliwa Kenya na kuchukua uraiya wa Ubeiljiji Divock Origi alifungia Ubeljiji bao la pekee na la ushindi dhidi ya Urusi katika mechi yao ya pili ya kundi H. Bao hilo la dakika za mejeruhi za mechi hiyo ndiyo iliyoiwezesha Ubeljiji kufuzu kwa mkondo wa pili wa timu kumi na sita bora.
Origi ambaye aliingia kama mchezaji wa akiba baada ya kuondoka kwa Romelu Lukaku alifuma bao hilo la kipekee kunako dakika ya 88 ya kipindi cha pili ya mechi hiyo alipopokea pasi nzuri kutoka kwa Eden Hazard . Ubeljiji ilikuwa tayari imeilaza Algeria mabao 2-1 katika mechi ya kwanza .

Awali Ubeljiji ilikuwa imemjaribu Igor Akinfeev ila mkwaju wake Kevin Mirallas ukagonga mwamba.
Ushindi huo uliiwacha Ubeljiji kileleni mwa kundi hilo wakiwa na alama 6 baada ya ushindi wao wa pili.
Wenyeji wa mashindano yajayo ya kombe la dunia mwaka 2018 Urusi watalazimika kufanya kazi ya ziada ilikufuzu kufuatia matokeo mawili ya kwanza huko Brazil
Lukaku; Ubeljiji 1-0 Urusi

Urusi ilikuwa imetoka sare na Korea katika mechi yao ya kwanza.
Hata hivyo Kocha Fabio Capello amesalia na mechi dhidi ya Algeria kujaribu bahati yake na mfumo mpya kabla ya kuabiri ndege ya Moscow.

Nchini Kenya ambapo Origi alikuza talanta yake ,wakenya wamemmiminia sifa kochokocho tineja huyo ambaye babake aliwahi kuichezea Harambee Stars .
Evelyn Wambui ‏kwenye tweeter alisema kuwa #Origi anaiwakilisha kenya katika kombe la dunia #TeamKenya in the #Worldcup2014 !
@kevojuice naye aliandika kuwa Origi ndiye mchezaji wa kwanza wa kenya kucheza kwenye kombe la dunia '' 1st Kenyan to score in World Cup...!!! #Origi hehe...
Na bbcswahili.

No comments:

Powered by Blogger.