Bao la kusawazisha la Silvestre Varela
Ureno ambayo ilikuwa imepata
pigo kubwa iliposhiindwa katika mechi yake ya ufunguzi na Ujerumani na
ilikuja katika mechi hii ikitafuta ushindi wa aina yeyote ilikuepuka
fedheha ya kufungashwa virago katika hatua ya makundi katika kombe la
dunia linaloendelea huko Brazil.
Kwa upande wao Marekani, ilikuwa inafahamu fika
kuwa matokeo baina ya 2-2 naina ya Black Stars ya Ghana na vinara wa
kundi G Ujerumani ilikuwa na hatari ya kuinyima fursa ya kushiriki
mkondo wa pili wa kombe la dunia kwa hivyo ilikuwa inatafuta ushindi
ambao ingeipa tiketi ya moja kwa moja katika hatua ijayo. Lakini kipenga cha kuanza kwa mechi hii kilpopulizwa, Nani ndiye aliyeiweka Ureno mbele baada ya dakika 5 ya mechi hiyo.
Ureno imejipata taabani baada ya kutoka sare ya 2 -2 na Marekani
Kuanzia hapo nipe nikupe baina ya mahasimu hao
wa jadi ikaendelea hadi dakika ya 64 Germaine Jones alipofaidi safu
tepetevu ya ulinzi na kuisawazishia Marekani. Vijana wa Jurgen Klinsmann ndiyo walionekana na
tamaa zaidi ya kushiriki mkondo wa pili wa kombe la dunia walipofaidi
kona iliyotokana na makosa ya Ricardo Costa na wakaitumia vyema.
Marekani ilifufua matumaini ya kusonga mbele
Clint Dempsey alipovurumisha mkwaju ndani ya neti na kuiweka timu yake
mbele , hata hivyo Christiano Ronaldo alimwandalia pasi nzuri na
akaisawazishia Ureno katika muda wa ziada wa mechi hiyo.
Ureno imejipata taabani baada ya kutoka sare ya 2 -2 na Marekani
Mwisho wa kuishia Ureno ilijizolea alama yake ya
kwanza katika kipute hicho huko Brazil lakini wanahitaji kuilaza Ghana
na kuomba kuwa Marekani wakunguwae dhidi ya ujerumani iliwao wafuzu
kusonga mbele.
Marekani inahitaji ushindi mkubwa dhidi ya Ujerumani ambayo itakuwa ikitafuta sare ya aina yeyote ilikusonga mbele.
Ghana kwa upande wao sasa wanahitaji kuichapa
Ureno na kuomba kuwa Ujerumani nayo itaitandika Marekani iliwafuzu kwa
mkondo ujao. Kufikia sasa ujerumai inaongoza kundi hili ikiwa na jumla ya ponti 4 sawa na Marekani.Ghana ni ya 3 na alama 1 sawa na Ureno.
Na bbcswahili.
No comments: