LIVE STREAM ADS

Header Ads

MICHEZO: MADAI YA UFISADI KATIKA SOKA YAIBUKA.



Kikosi cha soka cha Ghana

Shirikisho la soka nchini Ghana limewataka maafisa wa polisi kuingilia kati baada ya madai ya vyombo vya habari vya Uingereza kwamba mmoja wa maafisa wake alikubali timu ya nchi hiyo kucheza katika mechi zilizo fanyiwa ufisadi.

Mamlaka ya Soka nchini Ghana imekana madai ya jaribio lolote la kuuza mechi zake ama kuhusika kwa afisa yeyote katika ufisadi. Madai hayo yametolewa kufuatia uchunguzi wa pamoja kati ya gazeti la Uingereza la Daily Telegraph na Runinga ya Channel Four.

Katika taarifa yake shirikisho la soka duniani FIFA limesema kuwa hakuna ushahidi kwamba uadilifu wa michuano ya kombe la dunia umeathirika. Shirikisho la soka nchini Ghana limesema kuwa litamuekea vikwazo vikali afisa yeyote atakayepatikana na makosa hayo.
Na bbcswahili.

No comments:

Powered by Blogger.