Home
Unlabelled
PICHA ZA UTUPU MITANDAONI ZACHUKUA SURA MPYA. SERIKALI KUCHUKUA HATUA KWA WATAKAOBAINIKA. KUHUSU PICHA ZA UTUPU ZA MH.KOMBA NA WENGINEO SOMA HAPA KITAKACHOWAKABILI.
PICHA ZA UTUPU MITANDAONI ZACHUKUA SURA MPYA. SERIKALI KUCHUKUA HATUA KWA WATAKAOBAINIKA. KUHUSU PICHA ZA UTUPU ZA MH.KOMBA NA WENGINEO SOMA HAPA KITAKACHOWAKABILI.
Sakata
la kusambaa picha zisizokuwa na maadili mitandaoni zikiwemo za watu
maarufu hapa nchini leo limezungumziwa tena katika bunge la Tanzania
kule Dodoma ambapo katika kipindi cha maswali na majibu Mhe. Habib Mnyaa
ameonekana akihoji serikali inachukua hatua gani juu ya watu wanaotuma
picha zao zisizo na maadili mitandani zikiwemo za kina Wema na Diamond
wanazopiga wakiwa chumbani na kuweka kwenye mitandao.
Katika majibu yake waziri wa mawasiliano, sayansi na teknolojia Prof.
Makame Mbarawa anasema “Mhe. Spika kuhusu picha zisizokuwa na maadili
zinazowekwa katika mitandao na watu maarufu na hata wasiokuwa maarufu
serikali imeanza kuandaa kanuni zitakazokuwa zikifuatilia Online Content
ambapo itaanza kuchukua hatua baada ya kufuatilia juu ya picha hizo na
kuchukua hatua madhubuti”.
Baada ya kauli hiyo Spika wa bunge Mhe. Anne Makinda alikazia akitaka
majibu juu ya picha za juzi zilizosambaa zikimuonyesha Mhe. Komba akiwa
na binti mdogo ambazo mwenyewe alisema si zake na wabunge kuonekana
wakitaka majibu ambapo Mhe. Mbarawa anasema.
“Mhe. Spika kuhusu picha za juzi zilizosambaa mitandaoni tunazifuatilia
kujua zimeanzia wapi na taarifa zake zikoje kwani hata mimi bado
sijaziona ila tutachukua hatua tutakapobaini zilipotoka.”
Kwa ushirikiano na Millardayo.
PICHA ZA UTUPU MITANDAONI ZACHUKUA SURA MPYA. SERIKALI KUCHUKUA HATUA KWA WATAKAOBAINIKA. KUHUSU PICHA ZA UTUPU ZA MH.KOMBA NA WENGINEO SOMA HAPA KITAKACHOWAKABILI.
Reviewed by Anonymous
on
June 09, 2014
Rating: 5
No comments: