LIVE STREAM ADS

Header Ads

RAIS WA CHUO KIKUU BUGANDO NA MWENYEKITI WA VYUO VIKUU TANZANIA APATIKANA AKIWA HAJITAMBUI BAADA YA KUPOTEA KATIKA MAZINGIRA YA KUTATANISHA.



Pichani ni Mdede kabla hajatekwa
Rais wa chuo kikuu Bugando Mussa Leonard Mdede amepatikana usiku huu akiwa hajitambui na amepelekwa katika hospitali ya rufaa Bugando kwaajili ya vipimo na matibabu zaidi,bwana Mdede ambaye pia ni mwenyekiti wa TAHILISO nchini alitoweka tangia tarehe 18 mwezi huu saa kumi jioni,na haikuweza kufahamika mara moja yupo wapi na kama ametekwa nani kamteka, mpaka usiku huu taarifa za kupatikana kwake zilipotufikia.

Akiongea na mwandishi wa habari hii,waziri mkuu wa serikali ya wanafunzi Bugando Benjamini Thomas,alisema Mdede aliletwa na vijana watatu,wanaume wawili na mwanamke mmoja waliodai kumuokota bwana Mdede katika eneo la Usagala akiwa hajitambui wala kujielewa,
Anaendelea kusema kwa mujibu wa mama mwenye Nyumba wa Mdede,watu hao walidai baada ya kumuokota jana usiku katika eneo hilo la Usagala,waliamua kumchukua na kwenyda kumuhifadhi katika eneo la Igoma, alipoanza kupata fahamu na kueleza anaishi wapi ndipo wakamleta nyumbani kwake,huku watu hao wakidai walishindwa kumleta jana na asubuhi kutokana na Mdede kutojitambua na kuwa katika hali ya kupoteza kumbukumbu,hata hivyo mama  mwenye nyumba  anasema watu hao hawakukaa sana wakaondoka bila kutoa maelezo zaidi.


Waziri mkuu huyo wa Bugando aliendelea kusema, "kwa mujibu wa mama mwenye nyumba,alisema kwamba mara baada ya watu hao kumleta nyumbani hapo wakiwa wamempakia kwenye gari aina ya Kenta,walitoa maelezo machache na hawakutaka kukaa sana wakaaga wakaondoka ".
Kwa mujibu wa waziri mkuu Thomas anasema kaka yake alijaribu kuwapigia mara kadhaa lakini yeye hakupokea simu yake kwakuwa alikuwa anatoa tamko kwa waandishi wa habari juu ya kupotea kwa Mdede,na walipomaliza kutoa tamko walielekea kwa Mdede baada ya kuambiwa na kaka yake kila kitu,"na tulimkuta anamwonekano, anahali dhoofu,akiwa anaongea kwa tabu na huku akiwa hana kumbukumbu nzuri zaidi ya kumbukumbu ya kabla hajatekwa" 

Anaendelea kusema kuwa waliwasiliana na mkuu wa upelelezi wa wilaya ya Nyamagana na wakakubaliana wasitoe taarifa kwanza mpaka watakapo muhoji na kuangalia taratibu zingine za kiulinzi,na baadae ndipo walipojiridhisha na kuamua kumpeleka hospitalini Bugando kwani awali alikuwa akipatiwa matibabu palepale nyumbani kwake,lakini waliamua kumpeleka hospitali hiyo kwa ajili ya vipimo na uchunguzi zaidi na hasa walipoona hali ya Mdede haieleweki na wakahisi huenda akawa amelishwa vitu vibaya kama sumu.

Na: Nicholaus Kilunga

No comments:

Powered by Blogger.