TAHADHARI...UGONJWA WA EBOLA WAZIDI KUENEA KWA KASI KUBWA.
Shirika
la Afya Duniani (WHO) limetahadharisha juu ya uwezekano wa kuenea
ugonjwa wa Ebola barani Afrika. Msemaji wa WHO ameeleza kuwa, mlipuko wa
ugonjwa wa Ebola magharibi mwa Afrika ambao kwa mara ya kwanza
ulishuhudiwa katika mipaka ya nchi 3 za eneo hilo, unaripotiwa kuwa
uliyakumba maeneo mengi zaidi kijiografia toka ugonjwa huo ugunduliwe.
Ameongeza
kuwa, mlipuko huo haujaisha na kwamba kila siku kesi mpya zinaripotiwa
nchini Guinea, Sierra Leone na Liberia, kwa ajili hiyo nchi nyingine
zinatakiwa kuchukua tahadhari.
Wakati
huo huo Jumuiya ya Madaktari Wasio na Mpaka imetangaza kuwa, mlipuko wa
Ebola katika nchi za Guinea, Sierra Leone na Liberia haudhibitiki na
kwamba kuna hatari ya kuenea katika maeneo mengine.
WHO
imetangaza kuwa, ugonjwa huo umesababisha vifo vya watu 566 katika nchi
hizo 3 tangu ulipoanza huko Conakry mji mkuu wa Guinea. Dalili za homa
ya Ebola ni kuhara na kutapika sambamba na homa kali ambayo pia
huandamana na uvujaji mkubwa wa damu. Homa ya Ebola huambukizwa kwa
kugusa damu, jasho na kinyesi cha mtu mwenye ugonjwa huo.
No comments: