Kenny Salvatory (Kushoto), Alex Ngusa (katikati) na Mc.Katumba (Kulia) katika Studio za Metro FM.
Kuhusiana na Bajeti Tegemezi ambayo imekuwa ikilalamikiwa
hapa nchini, Dk.Kenny anasema kuwa hilo haliwezi kuepukika hata siku moja kwa hivi
sasa na hata katika siku za hivi karibuni (Zijazo) kwa kuwa asilimia kubwa ya
watanzania hawalipi kodi ikizingatiwa kwamba uchumi wa mataifa hutegemea kodi
kwa asilimia kubwa.
"Kwa Mfano chukulia kwamba Watanzania wanaopaswa kulipa kodi ni Milioni
25, Matokeo yake utakuta Watanzania Milioni Tano pekee ndio
wanaolipa kodi, sasa kwa hali hii lazima bajeti yetu itaendelea kuwa tegemezi
na Taifa litajikuta likiendelea kuongeza deni la Taifa kwa kuwa hakutakuwa na
namna ya kujinusuru zaidi ya kutegemea Wahisani na kuendelea kukopa. Na hii ndiyo ambayo imekuwa ikisababisha wafanyakazi Kila Siku kulalamikia Kodi kubwa wanayokatwa kwa kuwa asilimia kubwa wao ndio wanaolipa kodi”.
|
No comments: