LIVE STREAM ADS

Header Ads

DK.MAGUFULI KUZINDUA KIVUKO KIPYA JIJINI MWANZA. FOLENI SASA BYE BYE.



Wananchi na Wakazi wa Jiji la Mwanza wanatarajia Kuepukana na Usumbufu wa Foleni za Barabarani wanaokumbana nao hususani Majira ya Asubuhi na Jioni, Baada ya Waziri wa Ujenzi Dk.John Pombe Magufuli kutimiza ahadi ya Serikali kuleta Kivuko Jijini Mwanza kwa ajili ya kupambana na Foleni hizo.



Kivuko hicho ambacho kinatarajiwa Kuzinduliwa Kesho na Dk.Magufuli kitakuwa kikifanya Safari zake katika mwambao wa Ziwa Victoria kuanzia eneo la Luchelele Kupitia Sweya, Butimba, Mkuyuni, Igogo na hatimae Kirumba na hivyo kusaidia wananchi wa Jiji la Mwanza Kuepukana na Changamoto za Foleni za barabarani.



Taarifa kutoka Kitengo cha Mawasiliano, Wizara ya Ujenzi kwenda kwa Vyombo vya Habari zimeeleza kuwa Kivuko Hicho kitakuwa na uwezo wa Kusafiri kwa mwendo kasi, kwa lengo la kutoa huduma ya Usafiri kwa uharaka zaidi huku kikiwa na Uwezo wa Kubeba Tani 65 ambazo ni sawa na abiria 80 na Magari madogo matano kwa wakati Mmoja.



Japo bado gharama za Usafiri katika Kivuko hicho hazijawekwa wazi hadi pale kitakapozinduliwa Siku ya Kesho na Dk.Magufuli, Kivuko hicho kinatarajiwa kuwa Mkombozi kwa wananchi wa Jiji la Mwanza ambalo linakuwa kwa kasi kubwa na kusababisha Foleni kuanza kuwa kero kwa wasafiri wake kutokana na kutumia masaa mengi wakiwa barabarani wakati wa kwenda ama kutoka Makazini.



Kivuko hicho kitafahamika kwa Jina la MV.TEMESA na kitakuwa chini ya Usimamizi wa Wakala wa Ufundi na Umeme Tanzania (TEMESA), ambapo kesho TEMESA inatarajia kutangaza gharama za Usafiri katika Kifuko hicho huku Siku ya Kwanza baada ya Kuzinduliwa kwake Wananchi wakitarajia kutumia Kivuko hicho bure.

No comments:

Powered by Blogger.