Kwa Upande wa baadhi ya Wahitimu wa Mafunzo hayo wameelezea furaha
yao baada ya kuhitimu mafunzo ya Ulinzi yanayotolewa na Kampuni hiyo, kwa
kusema kuwa mafunzo hayo yatawapatia
fursa ya kujipatia ajira na hivyo kuondokana na tatizo la ajira ambalo lilikuwa
likiwakabili hapo awali kabla ya kupata mafunzo hayo.
Aidha wamewashauri vijana wengine kuchangamkia nafasi za Ulinzi zinazotolewa
na Kampuni ya KK.Security Kote nchini ili
kuweza kuondokana na Changamoto ya Upatikanaji wa ajira, kwa kuwa Kampuni hiyo
imekuwa ikichangia kwa sehemu kubwa katika kutoa ajira kwa Vijana huku
wakiahidi kuyatumia vyema mafunzo hayo kwa kuzingatia maadili ili kuimalisha
ulinzi na usalama katika jamii.
|
No comments: