Haya ni Mahafali ya Sita ya Kidato cha Nne katika Shule ya Sekondari Rebu iliyoko Kata ya Turwa Wilaya Tarime Mkoani Mara. Mahafali haya yalifanyika Mwaka jana October 18 katika Viwanja vya Shule hiyo. Ni Mahafali ambayo yalivuta hisia za wanafunzi wengi wa Shule hiyo ikizingatiwa kwamba wanafunzi waliohitimu Kidato cha nne Shuleni hapo Mwaka 2012 hawakuweza kufanya Mahafali yao kutokana na Sababu mbalimbali jambo ambalo lilifanya Mahafali haya kunoga zaidi kwa kuwa Wanafunzi wa Shule hiyo ni kama waliumizwa na kitendo cha Mahafali ya mwaka 2012 kutokufanyika. |
No comments: