LIVE STREAM ADS

Header Ads

USICHOKIJUA KUHUSU SHOW YA SERENGETI FIESTA 2014.




Dakika chache mara baada ya Ratiba ya Serengeti Fiesta 2014 kutangazwa Rasmi, Homa ya Show hiyo Kubwa Kabisa hapa nchini imetanda kila kona katika Mikoa ya Kanda ya Ziwa, hususani kwa wakazi wa wananchi wapenda burudani wa Jiji la Mwanza.


Muda mfupi tu mara baada ya Ratiba ya Serengeti Fiesta Kutangazwa hii leo kupitia Kipindi cha XXL Kinachorushwa na Clouds FM na Mwenyekiti wa kamati ya Fiesta 2014 Sebastian Maganga, nilipigwa na butwaa kwa wapenzi wa burudani niliokutana nao katika viunga vya Jiji la Mwanza ambao kila mmoja aliielezea show hiyo kwa mwonekano wa kuisubiri kwa hamu kubwa.


Kilichochsababisha pia nikapigwa na Butwaa ni pale wapenzi wa Burudani waliposhindwa kuficha hisia zao na kuonekana kufurahishwa na Ratiba za Fiesta 2014 kuanzia Kanda ya Ziwa ambapo show ya kwanza itapigwa katika Dimba la CCM Kirumba tarehe 09 Mwezi wa Nane mwaka huu (09.08.2014) kwa kiingilio cha shilingi 5,000 tu.


Siku moja kabla ya Kutangazwa kwa Show hiyo ya Fiesta (Jana Jumatano) Nilikutana na Baaadhi ya Wasanii wa Jiji la Mwanza,  kiukweli nilishangwa na namna kila mmoja alivyokuwa akinieleza kuhusiana na Serengeti Fiesta 2014. Wengi walinieleza namna ambavyo wamekuwa wakijifungia Studio ili kuhakikisha wanatoka na ngoma kali ambazo zitawapa nafasi ya kupanda katika Jukwaa la Fiesta 2014.


Baada ya Kuwasikiliza kwa Makini Wasanii hao, ndipo nikagundua Utofauti kati ya Shows zote ambazo zinapigwa hapa nchini. Kwanza kwa mapokeo tu ya wapenzi wa Burudani Jijini Mwanza na Kanda ya Ziwa kwa ujumla walivyoipokea Show hii, lakini pia namna ambavyo Wasanii wa Mwanza walivyonieleza kuwa wanaumiza vichwa ili kuhakikisha wanapata fursa ya kupanda katika Jukwaa la Fiesta Mwaka huu.


Kwa Mantiki hiyo, nadiriki kusema kuwa huu ndio utofauti kati ya Show ya Serengeti Fiesta na Shows zote hapa nchini ambapo  hii inaashiria kwamba shughuli yoyote ile katika jamii ni MAPOKEO. Kama shughuli ina mapokeo HASI katika jamii basi hiyo shughuli unaachana nayo na kuangalia shughuli nyingine ya kufanya ambayo itakuletea mapokeo CHANYA katika Jamii. 


Hadi kufikia hapa naweza kutamatisha kwa kusema kuwa SERENGETI FIESTA imeonyesha mapokea CHANYA katika jamii kwa maana ya wapenzi wa Burudani na Wasanii kwa ujumla hivyo ni jukumu la wahusika kuendelea kuiboresha Show hii ili imani ya wapenda burudani hapa nchini iendelee kuwepo ikiwa ni pamoja na wasanii wenyewe ambao tayari wamekuwa na Imani kwamba, wakipanda katika Jukwaa la Fiesta basi wanakuwa wamepiga hatua moja wapo kubwa ya Kimafanikio katika mziki wao.

HII NDIYO RATIBA KAMILI YA FIESTA 2014
 Na Mhariri: Mtanzania Media Blog.

No comments:

Powered by Blogger.