Watu wanne wa familia mbiili tofauti
wakazi wa mtaa wa Nyerere A, eneo la mabatini jijini Mwanza, wamefariki dunia
usiku wa kuamkia jana baada ya kuangukiwa na mawe wakiwa wamelala.
Tukio hilo limetokea majira ya saa
nane usiku, wakati mvua kubwa iliyoambatana na upepo mkali pamoja na radi
ilipokuwa ikinyesha.
Mwenyekiti wa serikali ya mtaa wa
Nyerere A, mabatini jijini Mwanza, Hassan Maulid amewataja waliofariki dunia
kuwa ni Sayi Otieno na Kwinta Kweko ambao ni mume na mke huku watoto wawili
Kelfine Masalu na Emanuel Joseph wa familia ya Bw.Joseph William nao pia
wakipoteza maisha, baada ya chumba walichokuwa wamelala kuangukiwa na jiwe
lililoporomoka kutoka juu mlimani.
Kaimu kamanda wa jeshi la Uokoaji na
Zimamoto Mkoa wa Mwanza Inspekta Augustino Magere amewashauri wakazi wa jiji la
Mwanza waishio maeneo ya milimani kuchukua tahadhari ili kuepusha maafa kama
yaliyojitokeza ikiwa ni pamoja na kuepukana na ujenzi katika maeneo ya milimani
ambayo ni hatarishi.
Chanzo: ITV
|
No comments: