Kamati ya Uzinduzi wa Meli ya MV, Jubilee Hope ikiongozwa na Askofu Mkuu wa Dayosisi ya Geita Askofu Mussa Magwesela (Wa tatu kutoka pande zote.)
Akitoa taarifa hii leo Mkoani Mwanza juu ya Mradi huo, Askofu wa Dayosisi
ya Geita Mussa Magwesela alieleza kwamba Mradi huo unatarajia kutoa huduma
mbalimbali za kimatibabu ambazo ni pamoja na Matibabu ya Meno, Matibabu ya
Mtoto, Mama na Uzazi sanjari na kutoa elimu na huduma kwa watu waishio na
maambukizi ya Virusi vya Ukimwi.
Aidha alibainisha kwamba mradi huo umekusudia kutekeleza shughuli zake
kwa Mfumo wa Meli ya Matibabu ambayo itakuwa ikizunguka katika Visiwa vya Ziwa
Victoria na kutoa huduma za Afya na Matibabu kwa wananchi wa Visiwa hivyo.
|
No comments: