BANK YA MKOMBOZI YAKABIDHI MSAADA KWA WATOTO YATIMA WA KIJIJI CHA MATUMAINI MWANZA.
Meneja wa benki tawi la Mwanza bwana Nichorus
Mokirya akitoa hotuba wakati wa kukabizi misaada katika kitu
cha watoto yatima cha Kijiji
cha Matumaini kilichopo Nyegezi, Jijini mwanza.
|
Banki ya Mkombozi
Tanzania imeendelea kurudisha sehemu ya
faida yake kwa kuwasaidia watoto
yatima wanaolelewa katika nyumba
ya kuwatunza watoto
yatima ya Kijiji cha Matumaini ilichopo Nyegezi, Wilaya ya
Nyamagana Mkoni Mwanza.
Akitoa hotuba fupi
jana katika hafla ya kukabidhi msaada wao kwa Kijiji hicho, Meneja wa Mkombozi tawi la Mwanza Bwana Nichorus Mokirya kwa niaba ya mkurugenzi mtandaji wa benki hiyo, alisema kuwa benki yake imeendelea na utaratibu wa kutoa sehemu ya faida yake kwa ajili ya kuisaidia jamii katika Nyanga ya elimu na kutoa kipaumbele kwa watoto wasio na wazazi au walezi yani yatima.
jana katika hafla ya kukabidhi msaada wao kwa Kijiji hicho, Meneja wa Mkombozi tawi la Mwanza Bwana Nichorus Mokirya kwa niaba ya mkurugenzi mtandaji wa benki hiyo, alisema kuwa benki yake imeendelea na utaratibu wa kutoa sehemu ya faida yake kwa ajili ya kuisaidia jamii katika Nyanga ya elimu na kutoa kipaumbele kwa watoto wasio na wazazi au walezi yani yatima.
Bwana Mokirya aliongeza kuwa Taifa lolote
ili liendeleaa linahitaji
watu wake kuwa na elimu, hivyo basi wao
kuwekeza katika elimu ni
maaamuzi sahihi kwao na
hawatajutia uamiuzi huo.
Aliwataja watoto watakaonufaika na msaada huo kuwa ni, Nacy
Osacar mwanafunzi wa kidato cha tatu, Kashuliza Kamugisha mwanafunzi wa kidato cha pili na
Peter Aklan mwanafunzi wa kidato cha kwanza, ambao wote wanasoma
katika shule ya Sekondari Twihulumile.
Pia bwana Mokirya alitoa rai
kwa wadau wengine
kuwa na desturi za
kuwasaidia watoto yatima
kwa kuwa hawana walezi na
wanaitegemea jamii inayowazunguka kuweza
kuwasaidia.
Benki ya Mkombozi
imekuwa itoa huduma
mbalimbali za kibenki na
hivyo basi faida wanayoipata
wanagawa sehemu ya faida
hiyo na kuirejesha kwa jamii
kupitia misaada ya
kielimu.
Naye Katibu wa Chama Cha
Waandishi wa Habari wa Kupiga Vita Matumizi ya Dawa za Kulevya na
Uhalifu Tanzania OJADACT, Dennis Mpagaze
alisema kuwa huduma
zinazotolewa na benki hiyo ni za
kiwango cha juu na
kinachowavutia watanzania wengi
kupata huduma za kibenki
katika benki hiyo, hali iliyopelekea hata chama
hicho kufungua akaunti
ya chama katika
benki hiyo.
Na:Edwin Soko.
No comments: