WATENDAJI WILAYANI TARIME WANAMUANGUSHA WAZIRI MAGUFULI.
Miezi michache tu baada ya ujenzi kukamilika, mifereji imeanza kumomonyoka kutokana na ujenzi wake kuwa katika kiwango hafifu hususani kutokana na uhaba wa theluji iliyokuwa inatumika. |
Kwanza
kabisa
napenda kupongeza juhudi zote zinazofanywa na Serikali katika
kuhakikisha kwamba barabara zote kuu hapa nchini hususani zinazounganisha
Wilaya moja na nyingine ama Mkoa Mmoja na Mwingine zinajengwa katika Kiwango
cha Lami.
Mara kadhaa
juhudi hizo zimekuwa zikichagizwa zaidi na Waziri wa Ujenzi Dk.John Pombe
Magufuli ambae mara kadhaa amekuwa akisisitiza zaidi juu ya kuhakikisha kwamba
barabara zote hapa nchini zinakuwa katika kiwango cha lami tena katika hali ya
ubora kwa ajili ya kusaidia katika shughuli mbalimbali za uzalishaji katika
Taifa.
Japo kwa
mwendo wa kusua sua kama wa Kinyonga, Wananchi wa Wilaya ya Tarime wakaanza
kuiona neema kutokana na Ujenzi wa Barabara ambayo asilimia kubwa ya Wananchi
wa Maeneo ya inje ya mji wa Tarime wanaitegemea kwa ajili ya kufikishia mazao
yao ya biashara sanjari na shughuli mbalimbali katika Mji wa Tarime.
Hapa
naizungumzia barabara ya Nyamwaga ambayo inaanzania katika mji wa Tarime na
kupita hadi katika Mji wa Nyamongo kuelekea hadi Mugumu Wilayani Serengereti
ikiwa ni barabara tegemewa sana kwa wananchi wa vijiji vingi sana Wilayani
Tarime kutokana na umhimu wake wa kuwaunganisha na mji wa Tarime.
Kwa
wasioijua vyema barabara hiyo ni kwamba, katika kipindi cha mvua huwa
haipitiki.Na pengine adha hiyo ndiyo iliyopelekea ujenzi wa kuiwekea barabara
hiyo kuanza ikiwa ni miaka kadhaa iliyopita nyuma ambapo imekuwa ikijengwa kwa
awamu kuanzia katika mji wa Tarime hadi sasa ambapo imefikia eneo Kibumaye
Kijiji cha Mogabiri.
Ukweli ni
kwamba barabara hiyo imekuwa ikijengwa kwa awamu tofauti tofauti huku mwonekano wake wa ubora ukiwa katika hali ya kufanana katika awamu zote ambazo imekuwa ikijengwa. Lakini kwa leo napenda nielezee ujenzi uliomalizika
hivi karibuni ambao ulianzia katika eneo la Rebu Centre na kuishia katika eneo
la Kibumae.
Ujenzi huo
naamini ulikuwa na wasimamizi (Watendaji) lakini ninachoweza kukisema ni kwamba
Watendaji hao wanamuaibisha Waziri mwenye dhamana ya ujenzi ambae ni Dk.John
Pombe Magufuli ambae siku zote amekuwa akisisitiza juu ya ujenzi wa barabara
tena zenye kiwango na ubora unaohitajika.
Kinyume na
matarajio hayo ya Dk.Magufuli, barabara hiyo ya Nyamwaga Wilayani Tarime katika
ujenzi wa kipande cha kuanzia Rebu Centre hadi Kibumaye, Mogabiri imejengwa kwa
kiwango cha kawaida sana, huku hali ikiwa mbaya zaidi katika ujenzi wa Mifereji ya
Maji machafu ambayo tayari imeanza kumomonyoka ikiwa ni miezi kadhaa tu tangu
ujenzi wake kukamilika.
Katika
kuzungumza na wananchi waliokuwa wanashuhudia ujenzi huo, wakaeleza kwamba ujenzi
huo hususani wa mifereji umekuwa katika hali ya kiwango cha chini kutokana na baadhi
ya watendaji wasio waadilifu ambao walipewa jukumu la kusimamia ujenzi wa barabara
hiyo kuingia katika biashara haramu ya kuuza mifuko ya theluji iliyokuwa
imenunuliwa mahususi kwa ajili ya ujenzi.
Hakika
nikapigwa na butwaa kutokana na kauli hiyo kutoka kwa baadhi ya wananchi
Wilayani humo.Na moja kwa moja wazo likanijia kwamba “BAADHI YA WATENDAJI
WILAYANI TARIME WANAMUANGUSHA WAZIRI MAGUFULI” hivyo wanapaswa kuona aibu kwa
kuwa sehemu ya kukwamisha juhudi za Waziri Magufuli katika ujenzi wa barabara
bora na zenye viwango vinavyokubalika.
TAZAMA PICHA
No comments: