LIVE STREAM ADS

Header Ads

TAARIFA YA OJADACT KWA WANAHABARI KUHUSU WASANII KUJIHUSISHA NA DAWA ZA KULVYA NCHINI.

NDUGU   WAANDISHI  WA  HABARI, CHAMA CHA WAANDISHI WA HABARI WANAOPIGA VITA MATUMIZI YA DAWA ZA KULEVYA NA UHALIFU (OJADACT)  KIMETOA  TAARIFA  HII  FUPI  KWA VYOMBO VYA  HABARI  BAADA  YA  WAANDISHI  WENGI
KUTAKA  KUJUA  NI “KWA NINI WASANII  WAMEKUWA  WAKIJIHUSISHA  ZAIDI  NA TUHUMA ZA  KUSAFIRISHA  NA KUTUMIA  DAWA ZA KULEVUA”?.

OJADACT  KWA MUDA MREFU  TUMEKUWA  TUKIFUATILIA TATIZO  HILI  NA HATIMAYE   KUAMUA KUTOA TAARIFA  HII  KWENU  BAADA  YA  KUFANYA  UCHUNGUZI    ULIOANZA MWANZONI MWA  MWAKA 2014.

BAADA  YA  TUKIO  LA  HIVI  KARIBUNI  LA KUSHIKWA  KWA BAADHI  YA WASANII  NA  DAWA ZA KULEVYA, TAASISI HII IMEKUWA  IKIPOKEA MASWALI  MENGI HUU YA MATUKIO  HAYO, HALI  ILIYOTUSUKUMA KUTOA  UTAFITI  WETU  KWA MUDA   HUU  KWENU ILI  KUWEZA  KUINUSURU  JAMII  NA JANGA  LA  DAWA ZA KULEVYA.

ZIFUATAZO NI SABABU  KUBWA  ZA WASANII/WANAMICHEZO  KUJITUMBUKIZA KWENYE  BIASHARA  YA MATUMIZI  NA USAFIRISHAJI WA DAWA ZA KULEVYA:

•UMAARUFU WAO  NA MVUTO  MBELE  YA WAFANYABIASHARA  WA DAWA ZA KULEVYA,  UNAWASHAWISHI  KUWATUMIA WASANII  KWA  AHADI   ZA KUWALIPA  MALIPO  MAKUBWA ILI WAENDELEE  KUWA MAARUFU NA KUWA NA MAISHA  MAZURI.

Kwa  kuwa  wasanii ni watu maarufu  na wenye  mvuto  kwa jamii, mara  nyingi wafanyabiashara  wa  dawa za kulevya  wanashawishika  nao  kutumia  kundi  hili ili kuweza kufanikisha  mambo yao  yaende  na  kuharibu  maisha  ya wasanii  hasa wanaposhikwa  na kuharibu   ndoto  zao.

•URAHISI  WAO WA KUPATA  VIZA ILI KUINGIA  NCHI ZA UGHAIBUNI  KWA LENGO LA  KUFANYA  MAONYESHO MBALIMBALI .

Wafanyabishara  wa dawa za kulevya  wanatumia mwanya wa  urahisi wa  kujenga  hoja ya  kusafiri   kama wasanii/ wanamichezo  kupata viza   za kwenda  kufanya  maonyesho Nchi za ughaibuni, kwani  kwa msanii  ni   rahisi  zaidi  kupata  viza hizo kuliko  mtu wa kawaida ambaye  ni  kazi  kujenga ushawishi huo.

•KIPATO  KIDOGO KWA WASANII  NA  MAISHA  YA  KIFAHARI.

Wauza  dawa za kulevya  wamekuwa  wakisoma alama za nyakati  kwa kubaini  wengi  wa wasanii  wamekuwa na kipato kidogo, huku jamii  ikiamini  wao ni mamilionea, hapo ndipo wafanyabiashara  hao  wanapotumia mwanya wa kuwarubuni  baadhi yao kuingia katika biashara  hiyo ili  waweze kuwa mamilionea  na kuishi maisha wanayofanana  na majina yao.

•KUTUMIA DAWA ZA KULEVYA KAMA  VICHANGAMSHI KATIKA MAONYESHO YAO (STIMULANTS) (PSYCHOLOGICAL DEPENDENCE).

Wasanii wengi   wanatumia  dawa za kulevya  kama  vichangamshi  katika  maonesho mbalimbali kwa lengo  la kuwavutia  wapenzi wao, hali  hiyo inawafanya  kuwa wategemezi  wa dawa za kulevya  na kuwafanya  kila  wanaposafiri  toka eneo  moja  kwenda eneo  jingine  lazima  wahakikishe wana dawa za kulevya. Hapo  ndipo baadhi  yao wanashikwa   na dawa hizo wakiwa  kwenye  vituo  vya  kusafiria (Viwanja  vya ndege, bandari  na mipaka  ya  nchi  kavu).

•UELEWA MDOGO   JUU  YA DAWA ZA KULEVYA.

–Jamii likiwemo  kundi hili la wasanii  halina uelewa na  tatizo la dawa kulevya  hasa  faida  na hasara zake, kwani  mwelekeo  umebaki  kuwa mmoja tu  yani  kutafuta  uchangamfu(Stimulants), vileta njozi/maruweruwe (Hallucinogens) na vipumbaza (Depressants) bila  kujali  madhara  yake  ya kimwili, kiakili na kiroho  sanjali  na utegemezi.

MAPENDEKEZO  YETU:

•ELIMU  KWA JAMII NZIMA  INAHITAJIKA  KUJENGA  UELEWA  WA DAWA  ZA KULEVYA.

Ni  vyema  sasa  jamii wakiwemo  wasanii  wakapata  elimu  tosha  ya  dawa  za kulevya  kwa kujua hatari  ya kujiingiza  kwenye  matumizi  ya dawa za kulevya  na madhara  yake  hasa  katika utegemezi.

•IANZISHWE  KAMPENI  MAALUMU KWA  WASANII.

Kampeni  hiyo  itasaidia  wasanii   kufundishwa  umuhimu  wao katika  Taifa  katika  kulinda  heshima  na Nchi  na uwakilishi mwema  katika Nyanja za kimataifa.

•SERIKALI  ITAZAME  NAMNA  YA KUSIMAMIA   HAKI ZA WASANII.

Endapo kazi za wasanii  zitasimama vyema  ni wazi  kuwa  wasanii watapata maslahi mazuri  ya kazi zao  na kuongeza kipato  chao  badala  ya sasa  kuibiwa  kazi zao  na kubaki na umaskini  hatimaye  kujihusisha na  biashara haramu ya dawa za kulevya.

NDUGU ZANGU WAANDISHI  UCHUNGUZI WETU NI MREFU  LAKINI  TUMETUMIA  KUONESHA  SEHEMU  NDOGO  TU  INAYOSADIFU  TATIZO  LA  SASA  ILI   KUWAPA HALI  HALISI  KWA MANTIKI YA  NINYI   KUIELIMISHA  JAMII   HII  WAKIWEMO  WASANII  WAJIEPUSHA  NA BIASHARA  HII.

Imeandaliwa  na OJADACT na Kutolewa na;

Edwinn Soko, Mwenyekiti 30/10/2014.

No comments:

Powered by Blogger.