LIVE STREAM ADS

Header Ads

MEYA WA JIJI LA MWANZA AWATAKA WANANCHI KUJIEPUSHA NA KAULI ZA WANASIASA AKIWEMO WENJE.

Mstahiki Meya wa Jiji la Mwanza Stanslaus Mabula amewataka wananchi wa Kata ya  Pamba na Jiji la Mwanza kwa Ujumla kutodanganyika na maneno ya wanasiasa ambayo hayalengi kuchochea maendeleo kwa wananchi.

Mabula ambae pia ni diwani wa Kata ya Mkolani Jijini Mwanza (CCM) alisema hayo
juzi wakati wa usimikaji wa kamanda mpya wa umoja wa vijana( UVCCM) Kata ya Pamba Rordrick Ngoye  na kuongeza kuwa chama cha mapinduzi kitaendelea kupuuzwa kotokana na watu wachache wanao kichafua kwa maslahi yao binafsi.

Alieleza kuwa vyama vya siasa vimekuwa vikiwadanganya wananchi kuwa wao ndio wameleta maendeleo na kukipinga chama kilichopo madarakani kwa madai kuwa hakileti maendeleo kwa wananchi wake.

Akimzungumzia  Mbunge Jimbo la Nyamagana Ezekia Wenje (CHADEMA), Mabula alieleza kuwa mbunge huyo amekuwa akijitapa kwamba Chama chake ndicho kimefanya juhudi  za ujenzi wa barabara za Karuta, Butimba Mkuyuni na Kiloleni huku akidai  wafanyabiashara ndio waliongoza kulipa kodi za ujenzi wa daraja la Mabatini, wakati ni jukumu la kila mfanyabiashara kulipia kodi hiyo.

“Kwa nini hakuthubutu kusema kuwa yeye ndio ameweka daraja la mabatini? badala yake alisema anawashukuru wafanyakazi kwa kulipa kodi na polisi kwa kuchangia kodi”alisema Mabula akinukuu kauli aliyoitoa Wenje hivi karibuni Mkoani wakati Rais Kikwete alipofanya ziara Mkoani Mwanza na hivyo kuwataka wananchi kujiepuka nae sanjari na kauli za namna hiyo.

Kwa upande wa Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Nyamagana Raphael Shilatu aliwasisitiza zaidi wananchi kuipigia kura katiba iliyopendekezwa pindi wakati wa kufanya hivyo utakapowadia ili kuweza kuleta maendeleo kwa wananchi wote kwani Katiba inayopendekezwa imetoa haki kwa kila mmoja.
Na:Prisca Japhes

1 comment:

  1. SIASA BWANA ZINA RAHA YAKE...LAKININ KWENYE SIASA HAPA NCHINI WOTE NI WALE WALE TU.HAWANA JIPYA.WOTE WALAJI TU.

    ReplyDelete

Powered by Blogger.