LIVE STREAM ADS

Header Ads

UFISADI WA ESCROW UNAUNGWA MKONO NA VIONGOZI WA SERIKALI.

Baadhi  ya  viongozi wa  kisiasa nchini  wamesema  sakata la  akaunti  ya  ESCROW  linaungwa  mkono  na baadhi  ya viongozi wa Serikali wasio waaminifu  wanaojilimbikizia  mali  huku  wakiliacha Taifa  likiwa maskini na wachache   wakijilimbikizia mali.

Hayo  yalibainishwa hivi karibuni Mkoani Mwanza na  Mbunge wa
Kigoma  Kusini  kupitia  NCCR  Mageuzi  David  Kafulila  na  Dokta  Hamis  Kigwagala, wakati  wa  mdahalo wa  wazi  ulioandaliwa  na  Chama  Cha  Waandishi wa Habari  za  Kupiga  Vita  Matumizi  ya Dawa za Kukevya  na  Uhalifu Tanzania (OJADACT).

Kwa   upande wake  kafulila  alisema  kuwa  sakata  la  akaunti  ya  ESCRO ni  ufisadi  mkubwa  unaofumbiwa  macho  na  baadhi  ya   viongozi  wenye  kunufaika  na fedha  hizo, huku wachache  walio na uzalendo  na  Nchi  wakionwa ni  wasaliti  kwa  kuwa  hawapo  tayari    kuingia kwenye  ufisadi  huo.

Kafulila  alieleza  hayo  mbele  wa  washiriki wa  mdahalo  na  kuongeza  kuwa sakata  hilo  ni  ufisadi  mkubwa  ambao  unaligharimu  Taifa, kwani  takribani fedha  Billioni  mia  nne  zimenyakuliwa  na wajanja wachache, ambapo  kimsingi  zingiweza  kusaidia  katika    kuboresha  maisha  ya watanzania.

Aidha Kafulila aliongeza kuwa serikali  isipowasilisha  ripoti  ya  uchunguzi  wa sakata  hilo  katika  bunge  lijalo, basi  yeye  ataanzisha kampeni  wa kuhamasisha  wananchi kudai  fedha  zao  kwa  kauli  mbiu  ya  “ Bring  Back   our  Money” yani  rudisheni   fedha  zetu.

Naye  Mbunge  wa Nzega Hamis Kigwangala  alisema kuwa, wapo   wabunge  wachache  ndani  ya  bunge ambao wanaamini kuwa watendaji wa wizara ya nishati  na madini wao ni miungu watu  ambao  hawawezi kufanya  makosa, matokeo  yake ni  kulindwa  kwa  ufisadi  kupitia  mikataba  yenye  utata ndani ya wizara  hiyo.

Kigwangala  aliongeza kuwa CCM sio  chama  kibaya  bali baadhi  ya  viongozi wake  ndio wabaya,  kwani  wamekuwa wakikiuka ilani  ya  chama  hicho  kwa lengo  la kujilimbikizia  mali na kuwaacha  watanzania  wakiwa maskini.

Kwa Upande wake Mwenyekiti  wa Chama Cha Waandishi wa  Habari wa Kupiga Vita Matumizi ya Dawa za Kulevya  na  Uhalifu  Tanzania  Edwin Soko, alisema kuwa  waliandaa mdahalo  huo ili kuwapa  nafasi wananchi kusikiliza nafasi  ya bunge katika  kulinda rasilimali za Taifa toka  kwa baadhi  ya wabunge  wa bunge  la  Jamhuri  ya Muungano wa Tanzania.


Soko  aliongeza  kuwa  OJADACT  wanapinga  uhalifu wa ukiukwaji wa katiba ya nchi  na sheria zilizopo unaofanywa na baadhi ya watendaji  pamoja  na wanasiasa wacheche kwa lengo la kujinufaisha wao wenyewe.
Na Mwandishi wetu-Mtanzaniamedia Blog.

No comments:

Powered by Blogger.