LIVE STREAM ADS

Header Ads

VIONGOZI NA WATALAAMU WA AFYA KANDA YA ZIWA WAKUTANA KUJADILI MRADI WA TIBU HOMA.

Washiriki wa Mkutano wa Viongozi wa Afya kutoka Mikoa ya Kanda ya Ziwa wakiwa katika Picha ya Pamoja na Mgeni Rasmi Dr.Neema Rusibamayila ambae ni Kaimu Mkurugenzi wa Huduma za Kinga kutoka Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii (Wa pili kutoka Kushoto waliokaa). Viongozi hao wamekutana hii leo Mkoani Mwanza kwa ajili ya Semna ya Siku mbili kuhusiana na Mradi wa Tibu Homa ambao unatekelezwa katika Mikoa ya Kanda ya Ziwa ukiwa na lengo la Kupunguza Maradhi na Vifo kwa Watoto walio chini ya umri wa Miaka Mitano kutokana na Magonjwa yanayosababisha Homa Kali kwa kuboresha ugunduzi wake na kutoa matibabu sahihi ya Magonjwa hayo. 

Mshirika Mkuu wa Mradi wa Tibu Homa
ni Shirika la University Research Co.,LLC (URC) kwa kushirikiana na Mshirika Mkuu Kitaifa ambae ni Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii pamoja na wadau wengine ambao ni Shirika la Amref for Health Africa, Management Science for Health (MSH) chini ya Ufadhili wa Shirika la Kimataifa la Maendeleo la Marekani (USAID) ambapo Mradi huo unatekelezwa katika Mikoa ya Kanda ya Ziwa ambayo ni Mwanza, Kagera, Mara, Shinyanga, Simiyu na Geita.
Washiriki wa Mkutano wa Viongozi wa Afya kutoka Mikoa ya Kanda ya Ziwa wakiwa katika Picha ya Pamoja na Mgeni Rasmi Dr.Neema Rusibamayila ambae ni Kaimu Mkurugenzi wa Huduma za Kinga kutoka Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii (Wa pili kutoka Kushoto waliokaa).Mkutano huo Umefanyika katika Ukumbi wa Hotel ya Malaika Beach Resort iliyopo Ilemela Mkoani Mwanza na unatarajia kufikia tamati kesho ijumaa.
Washiriki wa Mkutano wa Viongozi wa Afya kutoka Mikoa ya Kanda ya Ziwa wakiwa katika Picha ya Pamoja na Mgeni Rasmi Dr.Neema Rusibamayila ambae ni Kaimu Mkurugenzi wa Huduma za Kinga kutoka Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii (Wa pili kutoka Kushoto waliokaa).Mkutano huo Umefanyika katika Ukumbi wa Hotel ya Malaika Beach Resort iliyopo Ilemela Mkoani Mwanza na unatarajia kufikia tamati kesho ijumaa.
Kushoto ni Dr.Festus Kalokola ambae ni Mkurugenzi wa Ufundi wa Mradi wa Tibu Homa Kanda ya Ziwa, akifuatiwa na Dr.Neema Rusibamayila ambae ni Kaimu Mkurugenzi wa Huduma za Kinga kutoka Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii (Katikati) na wa Kwanza Kulia ni Dr.Samson Winani ambae ni Mganga Mkuu wa Hospitali ya Mkoa wa Mara.
Dr.Neema Rusibamayila ambae ni Kaimu Mkurugenzi wa Huduma za Kinga kutoka Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii.
Victor Masbayi ambae ni Mkurugenzi wa Mradi wa Tibu Homa unaoratibiwa katika Mikoa ya Kanda ya Ziwa.
Dr.Samson Winani ambae ni Mganga Mkuu wa Hospitali ya Mkoa wa Mara akizungumza katika Mkutano huo hii leo.
Baadhi ya Washiriki wa Mkutano huo.
Miongoni mwa Washiriki wa Mkutano huo.
Washiriki wa Mkutano wa Viongozi wa Afya kutoka Mikoa ya Kanda ya Ziwa wakiwa katika Semina juu ya Mradi wa Tibu Homa ambao unatekelezwa katika Mikoa ya Kanda ya Ziwa ukiwa na lengo la Kupunguza Maradhi na Vifo kwa Watoto walio chini ya umri wa Miaka Mitano kutokana na Magonjwa yanayosababisha Homa Kali kwa kuboresha ugunduzi wake na kutoa matibabu sahihi ya Magonjwa hayo.Mkutano huo Umefanyika katika Ukumbi wa Hotel ya Malaika Beach Resort iliyopo Ilemela Mkoani Mwanza na unatarajia kufikia tamati kesho ijumaa.
Na:George Binagi.

No comments:

Powered by Blogger.