LIVE STREAM ADS

Header Ads

HII YA MWIMBAJI WA MZIKI WA INJILI HAPA NCHINI JOHN LISU UMEINYAKA?

Mwimbaji wa Mziki wa Injili John Lisu.
Nina uhakika hii hujainyaka. Sasa kaa mkao wa Kusoma kile ambacho Mtanzaniamedia Blog imekuandalia baada ya kukinasa kutoka katika vyanzo vyake vya habari vinavyoaminika kote Ulimwenguni. Huu mchongo ni kuhusiana na Mwimbaji anaefanya vizuri kwa hivi sasa katika Mziki wa Injili hapa nchini akiwa anafahamika kwa jina la John Lisu.

Inshu yenyewe iko hivi,
Kwa wakazi wa Jiji la Mwanza na Viunga vyake, The Sound of Worship iliyopo JijinI Mwanza inawaletea Uko Hapa Tour itakayofanyika Jumapili ijayo ya Novemba 16, 2014 ndani ya Ukumbi wa Nyerere uliopo katika Hotel ya Gold Crest kuanzia saa nane Mchana ambapo Kwa kiingilio cha Shilingi Elfu Kumi tu (10,000) kwa Watu wazima na Shilingi Elfu Tatu tu (3,000) kwa watoto utapata kubarikiwa na mziki wa injili kutoka kwa Mwimbaji John Lisu.

Hakika hautakiwi kukosa burudani hii kutoka kwa John Lisu ambapo naamini utaweza kubarikiwa kupitia huduma hii ya uimbaji kutoka kwa John Lisu ambae pia atasindikizwa na kwaya na waimbaji mbalimbali kutoka ndani na nje ya Mkoa wa Mwanza.
Huu ndo Mpango Mzima.Kumbuka ni The Sound of Worship ndani ya Mwanza City akiwa anawaletea Uko Hapa Tour siku ya Jumapili ijayo ya Novemba 16, 2014 ndani ya Ukumbi wa Nyerere uliopo katika Hotel ya Gold Crest kuanzia saa nane za Mchana.Kwa kiingilio cha Shilingi Elfu Kumi tu kwa Watu wazima na Shilingi Elfu Tatu tu kwa watoto utapata kubarikiwa na mziki wa injili kutoka kwake Mwimbaji John Lisu.
Mwimbaji wa Mziki wa Injili John Lisu akitumbuiza katika moja ya Matamasha yake aliyowahi kuyafanya Mkoani Mwanza hivi karibuni ambapo kila mmoja aliewahi kuhudhuria katika Matamasha yake atakubaliana nami kuwa mtumishi huyu anajua kuitenda vyema huduma ya uimbaji aliyopewa na Mwenyezi Mungu.
Na:Jactan Msafiri.

No comments:

Powered by Blogger.