MAKALA: NYUMBA ZA UTIMAMU WA MWILI ZINASAIDIA WATEJA KUACHA DAWA ZA KULEVYA.
Uwepo wa
nyumba za utimamu wa mwili kwa
watumiji wa dawa za kulevya Nchini,
umesaidia kupunguza tatizo
la dawa za kulevya kwa
baadhi wa watumiaji
waliojitambua na kuwa tayari
kuacha dawa hizo
kwa kupata programu
maalumu zenye ushawishi wa kujitambua
na kuwa huru bila
kutumia dawa za kulevya .
Vituo
hivyo maarufu kama
Nyumba za utimamu wa mwili (rehabilitation centres
au sober houses)
zimekuwa vikitambulika na
serikali na kufanya kazi
chini ya miongozo
ya serikali. Nchini
Tanzania vituo hivi vinapatikana katika
mikoa mbalimbali ikiwemo, Tanga,
Dar es Salaam, Zanzibar , Arusha na
Mwanza, huku vikiwa na msaada mkubwa
kwa watumiaji wa dawa za kulevya
.
Nilitembelea moja ya kituo
hicho kinachojulikana kwa
jina la
Pili Misanah kilichopo
Pasiansi, Wilaya ya Ilemela
Jijini Mwanza na kukutana na meneja
wa kituo hicho, bwana
Mohammed Mohammed, ambaye aliniambia
shughuli zinazofanywa na
kituo hicho, zikiwemo
kuwahamasisha watumiaji wa dawa
za kulevya kuhudhuria mafunzo
ya kuacha kutumia
dawa za kulevya, kuwa na moyo wa kujitambua na kujikubali kuwa
wao ni watumiaji wa dawa za
kulevya na wanaweza kuishi bila
kutumia dawa za kulevya (Drug free)
na kutambua na kuvishinda vishawishi
vya dawa za kulevya.
Bwana
Mohammed alisema kuwa
mchango wa kituo
hicho ni mkubwa
sana katika jamii, kwani wateja
wengi wamekuwa wakiachana
na uteja kwa kupata mafunzo
ya namna ya
kuacha dawa za kulevya .
“Tulianza
kutoa huduma hizi
Februari, 2014 na watu
zaidi ya sabini wamepata huduma
hii na kati
ya hao arobaini wamepona
na kuacha kabisa kutumia
dawa za kulevya na
wanaendelea vyema na
shughuli za kujenga Nchi”, alisema Mohammed.
Pia
alisema kuwa programu ya
kumbadili mtu kutoka kwenye
matumizi ya dawa za kulevya na kuwa
msafi (Drug free),
inachukua muda wa miezi
sita kwa kufundishwa juu ya
kujikubali na kuwa tayari kuishi
nje ya maisha
ya matumizi ya
dawa za kulevya.
Naye
bwana Emmanuel Gofrey
aliyekuwa mtumiaji wa dawa
za kulevya na sasa amepona
kupitia kituo cha Pili
Missanah alisema kuwa, yeye
ameacha kabisa kutumia
dawa za kulevya na kwa sasa anafanya
biashara ya matunda
eneo la Kirumba
na anakishukuru sana kituo hicho
kwa kuwa mkombozi wa watumiaji wa
dawa za kulevya Jijini Mwanza.
Bwana
Lodrick Ngowi, mkazi wa
Mwanza alisema kuwa,
uwepo wa vituo
vya kutoa programu za
kuhamasisha watu kuacha
kutumia dawa za kulevya limesaidia sana
kwani, yeye kwa sasa anaishi na
kijana wake ambaye
ameacha kutumia dawa za
kulevya na amepona kabisa baada
ya kijana huyo
kupelekwa kwenye kituo
hicho.
Makala
hii pia ilibaini
changamaoto ya uwepo wa uingiaji kwenye
kituo hicho kwa waathirika wa dawa za kulevya wanaotaka huduma
ya kuacha dawa
za kulevya, kwa kukosa pesa
ya kulipia ambayo
ni shilingi laki
mbili. Kiwango hicho kimeonekana
kikubwa na
hivyo wanaoingia kituoni hapo
ni watu wenye
uwezo na wasio na uwezo
basi hawataweza kupata huduma
hiyo.
Kwa mujibu
wa Daktari Kasian Nyandidi wa
hospitali ya Muhimbili Jijini Dar es Salaam, alisema kuwa, baadhi
ya wateja wanaopata
huduma kwenye vituo
hivyo wamekuwa hawaachi
kabisa matumizi ya dawa za kulevya, kwani baadhi
ya tafiti zilizowahi
kufanywa kwa kuchukua sampuli
za haja ndogo
na kuzipima majibu
yameonyesha kuwa bado wanatumia dawa za kulevya huku
wakijitangaza kuwa wameacha
kutumia dawa na kuwa
huru.
Nyandidi aliongeza
kuwa ni vyema
kwa jamii ikatumia njia
zote za kusaidia watu
kuacha kuwa wateja
wa dawa za kulevya tofauti na kuamini
njia moja ambayo
inaweza kuwa na majibu tofauti, baadhi ya
njia zinazoweza kutumia ni
matumizi ya tiba
ya methadone ambayo
imeanza kutolewa kwenye hospitali
ya Mwananyamala, Muhimbili na
Temeke.
Yote
ya yote makala
hii imebaini kuwa
programu zinazotolewa katika
vituo hivyo zinaweza
kufanya kazi tu
endapo mhusika ataweza kujitambua na kuwa
tayari kubadilika na
kuacha dawa za kulevya,
kwani zinafundisha zaidi
mtu kujitambua na kuwa
msafi wa kiroho, kifikra na kimatendo
juu ya kuishi
huru bila matumizi ya dawa za kulevya.
Kwa ushauri wasiliana na Mwandishi wa makala
hii kwa simu 0754551306
Makala hii
imedhaminiwa na Mfuko
wa Kuvisaidia Vyombo vya Habari
Tanzania(TMF).
No comments: