SIKU YA WANAMKE DUNIANI MWAKA 2015 KUADHIMISHWA KIPEKEE JIJINI MWANZA.
Katika Kikao cha Pili cha Maadhimisho hayo kilichofanyika hii leo katika Ukumbi Mkubwa wa Mikutano wa
Halmashauri ya Jiji la Mwanza, Wadau mbalimbali kutoka Halmashauri ya Jiji la Mwanza, Vyombo vya Habari, Mashirika na Taasisi binafsi wakiwemo ambao wanaunda Kamati za Maadhimisho hayo wamekutana na Kujadiliana kwa pamoja namna ya kufanya ili Maadhimisho ya Siku ya Wanawake duniani yaweze kufanikiwa vyema.
Halmashauri ya Jiji la Mwanza, Wadau mbalimbali kutoka Halmashauri ya Jiji la Mwanza, Vyombo vya Habari, Mashirika na Taasisi binafsi wakiwemo ambao wanaunda Kamati za Maadhimisho hayo wamekutana na Kujadiliana kwa pamoja namna ya kufanya ili Maadhimisho ya Siku ya Wanawake duniani yaweze kufanikiwa vyema.
Mapendekezo mbalimbali yametolewa na Wadau hao, ambapo wadau mbalimbali wengine wameombwa kujitokeza kwa wingi kwa ajili ya Kushiriki katika Maadhimisho hayo ambayo Kilele chake kinatarajiwa kufanyika March Nane Mwaka huu katika Kata ya Mirongo ikiwa ni katika ngazi ya Wilaya ya Nyamagana (Jiji).
Siku ya wanawake duniani ilianza
kuadhimishwa mwaka 1911, wakati makundi ya wanawake nchini Marekani
yalipokusanyika kupinga udhalilishaji, ukandamizaji, uonevu na ubaguzi wa
kijinsia hususan katika sehemu za kazi.
Kuanzia wakati huo, Mataifa mbalimbali
yalianza kuadhimisha siku hiyo kwa lengo la kupinga mfumo dume ambao uliwabagua
wanawake kwa kuwanyima fursa za kusoma, kupata vyeo, mishahara mikubwa na haki
ya kushiriki katika shughuli za maendeleo kisiasa, kiuchumi na kijamii.
Vyama vya Wafanyakazi hapa nchini na
duniani kote wamekuwa mstari wa mbele katika maadhimisho ya siku hii, ambayo
kama nilivyotangulia kusema, kihistoria chimbuko lake limetokana na wafanyakazi
wanawake kupigania haki zao.
Siku hii inatoa fursa kwa wanajamii,
wafanyakazi wanawake, taasisi mbalimbali za Serikali na zisizo za kiserikali
kufanya tathmini juu ya masuala mbali mbali ya kimaendeleo kwa wanawake na hasa
kuangalia matatizo yanayowakabili na jinsi ya kuyatatua, kutafakari juu ya haki
zao katika ajira na jamii, kufanya tathmini juu ya mafanikio yao na kupanga
mikakati mipya ya kimaendeleo. Lengo kuu ni kuondoa vikwazo kwa wanawake katika
nyanja za kisiasa, kiuchumi na kijamii ili kujipatia maendeleo.
Aidha, madhumuni ya maadhimisho haya
ni kupima utekelezaji wa Maazimio, Matamko na Mikataba mbalimbali ya Kimataifa
inayohusu masuala ya wanawake.
Miongoni Mwa wadau Katika Jiji la Mwanza waliokutana leo katika Kikao cha pili cha Maandalizi ya Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani inayotarajiwa kuadhimishwa March Nane Mwaka huu |
Miongoni Mwa wadau Katika Jiji la Mwanza waliokutana leo katika Kikao cha pili cha Maandalizi ya Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani inayotarajiwa kuadhimishwa March Nane Mwaka huu |
Kulia ni Vervas Evodius kutoka Shirika la HAKIZETU akiwa na Winifrida Kaheshi (Kushoto) Kutoka Shirika la WOTESAWA Mkoani Mwanza. |
Miongoni Mwa wadau Katika Jiji la Mwanza waliokutana leo katika Kikao cha pili cha Maandalizi ya Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani inayotarajiwa kuadhimishwa March Nane Mwaka huu |
Kushoto ni Dicksoni Sija Kutoka Shirika la NACOPH akiwa pamoja na Rahel Zakayo (Kulia) kutoka Shirika la ACORD. |
Miongoni Mwa wadau Katika Jiji la Mwanza waliokutana leo katika Kikao cha pili cha Maandalizi ya Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani inayotarajiwa kuadhimishwa March Nane Mwaka huu |
No comments: