BWANA RAPHAEL NYAMASATI WA TARIME MKOANI MARA KUFUNGA NDOA NA BI.HILDA WA MAGENA TARIME.
Na: George Binagi-GB Pazzo
Kwa
Heshima na Taadhima, Bw.Rafael Francis Ryoba Nyamasati Mkazi wa Kijiji cha Kenyamanyori
Wilaya ya Tarime Mkoani Mara, kwa Kushirikiana na Kamati yake ya Maandalizi ya Harusi, anapenda kukukaribisha/ kuwakaribisha ndugu, jamaa na
marafiki katika harusi yake inayotarajiwa kufanyika Mwezi huu.
Harusi hiyo inatarajiwa kufanyika alhamisi Wiki ijayo ya tarehe 12.03.2015 Kijiji katika cha
Kenyamanyori Wilaya ya Tarime Mkoani
Mara, ambapo Bw. Rafael Francis Ryoba Nyamasati anatarajiwa siku hiyo kufunga ndoa na Bi.Hilda Mkazi wa
Kijiji cha Magena Tarime Mkoani Mara.
Kwa niaba ya Bwana Harusi pamoja na Kamati yake ya Harusi, Familia
ya Mzee Ryoba Nyamasati inayofuraha
kubwa kukukaribisha katika harusi hiyo, kwa maana kushiriki kwako ndiyo furaha
na mafanikio katika
harusi hiyo. Nyote Mnakaribishwa Sana.
Binagi Media Group, Kwa Pamoja Tuijuze Jamii
tunapenda kuwatakia Maandalizi Mema ya Harusi hiyo.
KUWA WA KWANZA KUWEKA HABARI/ TUKIO LAKO KATIKA MTANDAO HUU. MAWASILIANO: 0757 43 26 94.
No comments: