LIVE STREAM ADS

Header Ads

MVUA MKOANI SHINYANGA YASABABISHA MAAFA MAKUBWA. VIFO PIA VYATOKEA.

Miongoni mwa Nyumba zilizobomolewa Wilayani Kahama Mkoa wa Sinyanga kutokana na Mvua ya Mawe iliyonyesha Usiku wa Kuamkia leo March 04, 2015 na Kusababisha vifo vya Watu zaidi ya 38 huku wengine zaidi ya 60 wakijeruhiwa. Pia mvua hiyo imesababisha uharibifu wa mazao pamoja na mifugo kufariki. Wananchi wengi pia wamekosa makazi kufuatia mvua hiyo. 
Mvua hiyo ambayo ilinyesha kwa muda mfupi imewaacha watu 3,500  bila makazi katika kaya 350 huku nyumba zikifurika maji na baadhi ya mifugo ikisombwa.

Mkuu wa mkoa wa Shinyanga Bw. Ali Nasoro Rufunga amesema mvua hiyo ya mawe iliyoambatana na upepo mkali ilisababisha mafuruko katika kata ya Mwakata kuezua nyumba na nyingine kuanguka.

Amesema mali mbalimbali zimeharibiwa vibaya ikiwemo mifugo kuzolewa na maji na vyakula kwenye eneo lote lililokumbwa na mafuriko hayo.

Hali ya majeruhi ambao wamepelekwa katika hospitali mbalimbali bado sio nzuri kwa baadhi ingawa wengine wanaendelea vizuri.
Hali halisi ilivyokuwa Wilayani Kahama Mkoani Shinyanga Kufuatia Mvua kubwa iliyonyesha Usiku wa Kuamkia leo jumatano March 04, 2015 na Kusababisha Maafa makubwa. Mvua hiyo iliambatana na Upepo mkali sanjari na Mawe pia.
Baadhi ya Mifugo iliyopoteza maisha kutokana na Mvua Kubwa iliyonyesha Mkoani Shinyanga Usiku wa Kuamkia leo march 4, 2015 huku ikiwa imeambatana na Mawe na hivyo kusababisha maaafa makubwa.
Baadhi ya Wananchi waliopoteza Maisha baada ya nyumba zao kuanguka kutokana na Mvua Kubwa iliyonyesha Usiku wa Kuamkia leo March 04, 2015 Mkoani Shinyanga Wilaya ya Kahama huku ikiwa imeambatana na mawe.
BINAGI MEDIA GROUP, TUNATOA POLE KWA NDUGU, JAMAA NA MARAFIKI WALIOPATWA NA MAAFA HAYA.
PICHA KWA HISANI YA WADAU WAKIONGOZWA SEFU KULUNGE.

No comments:

Powered by Blogger.