LIVE STREAM ADS

Header Ads

NIYONZIMA KUUKOSA MCHEZO DHIDI YA YANGA NA ETOILE DU SALEH JUMAMOSI.

Genya Richard Mchambuzi wa Michezo
Na:Genya Richard
Kiungo mahiri wa klabu ya yanga Haruna Niyonzima amezuwa wasiwasi mkubwa klabuni hapo baada ya kuwepo taarifa kuwa kiungo huyo huenda akaukosa mchezo kati ya timu na Etoile du Sahel kutoka nchini Tunisia katika mchezo wa kombe la shirikisho barani Afrika siku ya jumamosi katika uwanja wa Taifa Jijin Dar es laam unaotarajiwa kuchezwa majira ya saa tisa alasiri.

Daktari wa misuli katika klabu hiyo Jackobo Onyango ambaye alitumia muda wa dakika kumi kumtibu misuli Niyonzima alisema kuwa hali ya Mchezaji huyo inaendelea vyema na kuna uwezekano mkubwa wa kucheza mechi hiyo siku ya jumamosi.

Wakati huo huo tayari Watunisia hao wameisha wasili nchini kwa ajili ya pambano hilo ambapo msemaji wa klab hiyo ya Etoile du Sahel Musitafa amesema kuwa timu hiyo imejiandaa vizuri kwa ajili ya mchezo huo huku akisisitiza kuwa lazima Yanga ikione cha mtema kuni siku ya pambano hilo.

HISTORIA YA ETOILE du SAHEL
Ikumbukwe kuwa Etoile du Sahel ni timu kongwe hapa Barani Afrika  kwani ilianzishwa May 25 mwaka 1920 na mpinzan wake mkuu ni timu ya Espearance du Sportivu. Etoile imeisha chukua kombe la shirikisho barani Afrika kwa miaka miwili ambapo mara ya kwanza kuchukua kombe hilo ilikuwa mwaka 1997 na mara ya pili ikiwa ni mwaka 2003.

Mwaka 1950 klabu hii ilichukua ubingwa wa ligi ya Tunisia  kwa mara ya kwanza ambapo tayari ambapo imekwisha nyakua ubingwa wa ligi hiyo mara tisa huku sifa kubwa ya timu hiyo ikiwa ni kujua kupoteza muda pindi inapokuwa uwanjan kwani hutumia asilimia zaidi ya 50 kucheza na waamuz kisaikolojia kwa kulalama na kumtaka refa kutoa adhabu iwe penati ama faulu.

 Pia ni wapigaji wazuri wa mipira iliyokufa [balldied] ambapo Waarabu hao hutumia asilimia zaidi ya 20 kucheza mpira uwanjan kwa dakika 60 ama 70 kwa kucheza mchezo ambao ni viding game yaan wakiwa ni watu wanaopenda kujirusha sana tena wakitumia ujanja wao kumtaka refa kuwabeba .

Hivyo Yanga inawabidi kuwa makini na Waarabu hao ambao wanajua sana fitina katika soka na inabidi Yanga siku hiyo icheze nao kisaikolojia vinginevyo safari yao itabaki kuwa hadithi ya soka la Tanzania kuwa “tutajipanga msimu ujao tena tukionekana kuwatupia lawama waamuzi ama ubovu wa viwanja”.
USHAURI: genyarichard@gmail.com
0713208878
                                                                     BINAGI MEDIA GROUP PRODUCTION

No comments:

Powered by Blogger.