BINAGI RADIO: CHAMA CHA MAPINDUZI CCM MKOANI MWANZA CHAANZISHA UTARATIBU HUU.
Katibu wa CCM Mkoa wa Mwanza Miraji Mtaturu (katikati wenye kofia) akiwa pa moja na Katibu wa CCM Wilaya ya Nyamagana Elias Mpanda (Kulia wenye kofia) wakiwa pamoja na washiriki wengine wa Mazoezi hii leo.
Na:George GB Pazzo
Katika kukabiliana na Changamoto za
Kiafya zinazosababishwa na Magonjwa mbalimbali, wananchi wa rika zote Jijini
Mwanza wametakiwa kufanya mazoezi ya viungo kwa lengo la kujiweka katika Afya iliyo
bora.
Hayo yamesemwa
na Katibu wa Chama cha Mapinduzi CCM Mkoani Mwanza Miraji Mtaturu, wakati wa
Mazoezi ya Viungo yaliyoanza hii leo kwa kuwashirikisha wananchi wote chini ya
Uratibu wa chama hicho.
Mtaturu
amesema kuwa watu wengi wamekuwa wakipata matatizo ya kiafya huku wengine
wakipoteza maisha kutokana na kutofanya mazoezi, hivyo hali hiyo si vyema
ikaachwa iendelee ambapo amewasihi watu wote bila kujali rika zao kujiunga kwa
pamoja kwa ajili ya Kushiriki katika Mazoezi.
Amebainisha
kuwa utaratibu huo wa kufanya mazoezi ya viungo utakuwa ukifanyika kila siku ya
Jumamosi kuanzia saa kumi na mbili kamili za asubuhi ambapo mazoezi hayo yatakuwa
yakitanguliwa na zoezi la kukimbia ambapo mbio zitakuwa zikianzia eneo la Gand
Hall Jijini Mwanza.
Miongoni mwa
Walioshiriki mazoezi hayo ambao ni pamoja na Jesca Mbogo, Neema Deogratius
pamoja na Ahmed Waziri Gao ambae ni Mwenyekiti wa Timu ya Soka ya Toto Africa
ya Jijini Mwanza, wamekipongeza Chama cha Mapinduzi CCM kwa kuanzisha utaratibu
huo wa Kufanya Mazoezi kila Jumamosi, kwa kuwa hatua hiyo itasaidia kuweka afya
za wananchi katika hali bora na nzuri kiafya na hivyo kuwaepusha na magonjwa
yasiyotarajiwa.
Wataalamu
mbalimbali wa Afya wamekuwa wakihimiza umuhimu wa mazoezi kwa kuwa mazoezi
husaidia kuweka mwili wa mwanadamu katika hali nzuri kiafya na hivyo kumsaidia
kuondokana na unene uliopitiliza lakini pia kujiepusha na magonjwa kama vile
presha ikiwa ni miongoni mwa magonjwa mengine mengi.
BONYEZA PLAY HAPA CHINI KUSIKILIZA BINAGI RADIO
Mbio zikiendelea
Mtaa kwa Mtaa
Mbio zikiendelea
Mazoezi ni mhimu sana
Mazoezi ya Viungo katika Uwanja wa Serengeti Mirongo Jijini Mwanza.
Mazoezi ya Viungo yakiendelea
Hapa watu wa...na...pu...mu..aaaa jeeeee
Katibu wa CCM Mkoa wa Mwanza Miraji Mtaturu
Ahmed
Waziri Gao ambae ni Mwenyekiti wa Timu ya Soka ya Toto Africa ya Jijini Mwanza alikuwa ni miongoni mwa walioshiriki mazoezi hii leo.
Neema
Deogratius miongoni mwa washiriki
No comments: