LIVE STREAM ADS

Header Ads

JIJI LA DAR ES SALAAM LAZIZIMA KUTOKANA NA MAFURIKO...SABABU ZATAJWA.

Na:Kennysalfes Salvatory-Dar es Salaam
Jiji la dar es salaam ndilo jiji linalotajwa kuwa na idadi kubwa ya watu nchini. Duru za takwimu kwa mujibu ya sensa ya mwaka 2012 zinataja idadi ya watu kufikia Milioni  Tano ikiwa ni ongezeko la asilimia 12 kutoka sensa za miaka ya nyuma.

Hapana shaka tangu mwezi huu  wa Mei uanze ukimuuliza mtu yeyote swali hili,"KATI YA JUA NA MVUA BORA NINI?"...Wote watakujibu ...BORA JUA! Hii ni kutokana na mwendelezo mkubwa wa mvua za masika zinazoendelea hapa na maeneo mengine yote ya ukanda wa pwani ikiwemo Tanga, Tanzibar Lindi na kwingineko na hivyo kusababisha Shughuli nyingi hususani za uzalishaji,huduma za kijamii na nyinginezo nyingi kusimama.

Hii inatokana na miundombinu ya usafirishaji ikiwemo barabara na madaraja kuwa katika hali tete ambapo maji yamefurika barabarani, madaraja yamevunjika kiasi cha kulazimisha kikosi cha usalama barabarani kuzifunga baadhi ya barabara kwa usalama wa raia na mali zao.

Kwa mujibu wa mamlaka ya hali ya hewa nchini, imeelezwa kuwa sababu kubwa za mvua zinazoendelea kunyesha katika maeneo mbalimbali ya Ukanda wa Pwani hapa nchini ni kutokana na KUWEPO KWA MGANDAMIZO MDOGO WA HEWA.

Katika maelezo yake Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka hiyo Dr.Agness Kijaz, mvua hizo zinatazamiwa kuendelea kunyesha hadi mwishoni mwa mwezi huu huku ikielezwa kuwa  kiwango cha mvua kinaweza kuongezeka hadi kufikia Mm 50 kwa masaa 24 kikiwa ni kiwango cha juu zaidi na mvua kubwa katika kiwango hicho ambapo awali mvua hiyo ilitegemewa kunyesha tarehe  6 na 7 mwezi huu na hivyo ndivyo ilivyokuwa.

Dr.Kijazi alibainisha kuwa kiwango cha mm 20 kwa saa 24 kitaendelea hadi tarehe 18 ya mwezi huu hivyo ni vyema tahadhari mbalimbali zikaendelea kuchukuliwa ili kuondokana na madhara ambayo yameanza tayari kujitokeza ikiwa ni pamoja na Uharibifu wa Miundominu.

Tayari Madaraja kadhaa yameripotiwa kuvunjika likiwemo lile la Mbagala Kuu-Kibichi na mengine ya Kinondoni, Barabara kujaa maji, Vitu, mali na biashara za wananchi kusombwa na maji, shule kusitisha masomo huku athari kubwa zaidi ni ya vifo vya takribani watu wanane ikiwa imeripotiwa kutokea jijini Dar es salaam.

kwa mujibu wa taarifa zilizothibitishwa na mamlaka ya utawala mpaka asubuhi hii,jumla ya watu wanane wakiwemo wanawake wa 3 na wanaume watano akiwemo mtoto mwenye umri wa mwaka mmoja wameripotiwa kufariki dunia huku duru zikidokeza kuwepo kwa madhara mengine makubwa Jijini hapa.


Baadhi ya watalaamu wamekuwa wakieleza kuwa Miundombinu ya Jiji la Dar es salaamu imeelemewa jambo ambalo limekuwa likisababisha athari ya mafuriko kuwa kubwa zaidi Jijini hapa. Kwa kuwa mimi si mtalaamu wa masuala hayo, naomba kuisihi Serikali kama hoja hiyo ina ukweli ndani yake basi ishughulikiwe ili kunusuru madhara ya mara kwa mara ambayo hutokana na mvua zinazonyesha katika vipindi tofauti tofauti. Lakini pia kwa ndugu zangu wanaoishi mabondeni, nao ni vyema wakachukua hatua mapema na kuondoka katika maeneo hayo kwa kuwa wao ndio waathirika wa kwanza wakati wa mafuriko.

No comments:

Powered by Blogger.