LIVE STREAM ADS

Header Ads

UMOJA WA ULAYA KUENDELEA KUIKOMALIA SERIKALI YA TANZANIA.

Meza kuu katika maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Habari Duniani. Kutoka kushoto ni  Makamu wa Rais wa Umoja wa Vilabu vya waandishi wa Habari nchini (UTPC), Jane Mihanji, Mkurugenzi wa Mfuko wa Vyombo vya Habari Tanzania (TMF), Bw. Ernest Sungura, Balozi wa Umoja wa Ulaya (EU) nchini Filiberto Sebregondi na Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro Rodriguez.
Na:Edwin Soko
Jumuiya ya  nchi  za  Ulaya  imesema kuwa  itaendelea  kupaza sauti yake  kwa  serikali ya  Tanzania  katika  kulinda  na  kuheshimu haki za binadamu, ikiwemo uhuru wa vyombo vya  habari pamoja na haki ya  kupata  habari  ili kuchochea  kukua  kwa  maendelea  ya kidemokrasia Nchini.

Hayo yalisemwa na balozi wa  umoja wa  ulaya  Nchini Tanzania Filibero  Ceriansebregondi  alipokuwa  anafungua  rasmi  kilele   cha  maadhimisho  ya siku  ya  Uhuru wa  Vyombo  vya  Habari Duniani kwa  mwaka huu yaliyofanyika  Mkoani Morogoro.

Ceriansebregondi   alibainisha  kuwa   uwakilishi wake  Nchini  Tanzania  utalenga kufanya  mashauriano  na serikali  juu ya  kuheshimu  uhuru  wa  vyombo  vya  habari na  haki  ya  kupata   habari kwa kuwa ni nguzo muhimu  kwa  Nchi  yoyote  katika kupata  maendeleo popote duniani.

Naye  mratibu wa  umoja  wa  ulaya  Tanzania Alvero  Rodriguez   alisema  kuwa, huu ni  mwaka  muhimu sana kwa  Tanzania na jumuiya  za kimataifa, kuhakikisha  nafasi  ya  waandishi wa  habari inapewa thamani yake hususani katika shughuli za uchaguzi mkuu.

Rudriguez  alibainisha  kuwa jukumu  hilo  kwa  waandishi  lazima  lifuate  maadili  ya  uandishi wa habari  kwa kuhakikisha  kuwa  haki na  usawa pamoja  na  ulinganifu wa habari unazingatiwa, pamoja na watawala  kutoweka  sheria  nyingi zenye kukandamiza  uhuru wa  vyombo  vya  habari.

Naye  mwenyekiti wa wa taasisi  ya  vyombo  vya  habari  kusini mwa jangwa la Sahara   Saimon  Berege   alisema  kuwa  Tanzania  imeporomoka  katika  viwango  vya kimataifa  vya   kulinda  na kuheshimu  uhuru wa  vyombo vya  habari.

Berege  alisema  kuwa, kwa mujibu wa  taasisi  ya  waandishi wa    habari wasio na  mipaka  Tanzania  imeshika  nafasi  ya 75  duniani    kwa kuheshimu  uhuru wa vyombo  vya  habari  hadi  kufikia  mwezi  April, 2015  toka  nafasi  ya  69  kwa mwaka 2014.

Barege  alisistiza  kuwa  hiyo  yote  inatokana  na uwepo wa  mazingira  mabaya  ya  kulinda  uhuru wa  vyombo  vya  habari hapa Nchini  ikiwemo  kutungwa  kwa sheria  mbaya na  kandamizi  kwa  vyombo  vya  habari, vitisho  na  vipigo  kwa baadhi ya waandishi.

Pia  alisisitiza  kuwa, inasikitisha  kuona  Nchi  yenye  magazeti  zaidi  ya 800 redio zaidi  ya 100  lakini  Nchi  hiyo  hiyo  inatunga  sheria  mbaya  zenye  kukandamiza  vyombo  vya  habari.

Kwa upande wake wenyekiti wa  jukwaa  la wahariri  Tanzania  Absalom Kibanda  alisema  kuwa, kimsingi  maadhimisho  ya mwaka  huu  yanahitimisha  miaka 10  ya  unyanyaswaji wa  tasnia  ya  habari  kuliko awamu  zote  za uongozi zilizopita, kwani  serikali  inayomaliza  muda  wake  ndiyo  iliyokiuka  kwa  kiasi  kikubwa  uhuru  wa vyombo vya  habari, kwa  kuuawa  kwa  mwanahabari Daud Mwangozi, kujeruhiwa kwa baadhi ya waandishi wa Habari na kutungwa kwa sheria  mbaya  na kandamizi  ikiwemo sheria  ya  takwimu na makosa  ya  mtandanioni.

Maadhimisho  hayo  yalienda sanjari na mada  mbalimbali  na kufuatiwa  na  ushuhuda  wa  waaandishi wa  habari  waliowahi  kupata  maswahibu  katika    tasnia  ya  habari  , akiwemo  Josephat  Isango aliyekuwa  mwandishi wa  gazeti  la Tanzania  Daima,   Maxence  Melo mmiliki wa mtandao  na  jamii  forum na  Majjid Mjengwa  mmiliki wa  blog  ya mjenjwa .

Kilele cha Maadhimisho  ya Siku  ya  Uhuru wa  Vyombo  vya  Habari Duniani kilifanyika May Mbili ambapo Kauli  mbiu  yake ilikuwa inalenga juu ya Usalama  wa Habari  katika  dhama  za Dijitali, uandishi bora, usawa wa kijinsia  na faragha.

No comments:

Powered by Blogger.