LIVE STREAM ADS

Header Ads

MKURUGENZI MTENDAJI WA ASMENT AWAFUNGUKIA WAKURUGENZI WA RADIO ZA KIJAMII NCHINI.

Na:Prisca Mshumbuzi
Wamiliki wa Radio za Kijamii wametakiwa kujenga taswira njema katika Radio hizo ikiwa wanahitaji ziwavutie wasikilizaji wake pamoja na wadau mbalimbaliwa maendeleo hapa nchini.

Rai hiyo ilitolewa wiki hii Mkoani Mwanza na mwezeshaji wa warsha ya viongozi wa Radio za Kijamii ambae pia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Asasi ya kuwawezesha wajasiriamali wadogo na wa kati (ASMET) Ramadhan Ahung.

Ahung alieleza kuwa malengo ya warsha hiyo na madhumuni yake ni kuwepo kwa mpango wa biashara ndani ya redio hizo hakutakuwa na maana kama wasipozingatia ujenzi wa taswira utakaofanywa na wadau kuvutiwa na redio hizo.

“kitu kinachowavutia wasikilizaji ni namna ya kupanga taswira ya Vipindi na namna ya kuvitangaza kwa mvuto ambapo jamii kwa ujumla itavutiwa kuvisikiliza kila siku katika hizi Radio.” Alisema Ahung.

Aidha Ahung alisema kuwa kuna umuhimu wa Radio za Kijamii pia kuzingatia mahusiano bora kati yake na wanajamii, watu binafsi pamoja na taasisi za kiraia zenye malengo tofauti tofauti ambapo alisema hatua hiyo itasaidia radio hizo kuimarika kibiashara zaidi pia.

“Mahusiano mazuri ndio msingi wa kuleta maendeleo katika jamii, tofauti na hapo kunaweza kusababisha marumbano ambayo hayawajengi wanajamii na hivyo mwisho siku Radio za Kijamii zitaangukia pabaya” Alisema Ahung.

Warsha hiyo ilikuwa ikihitimisha awamu ya kwanza kwa ufadhili wa mradi wa shirika la maendeleo la Sweden (SIDA) wa kuzipa uwezo Radio za Kjamii katika matumizi ya Tehama chini ya uratibu wa shirika la kimataifa la elimu sayansi na utamaduni UNESCO iliyofanyika katika kituo cha Radio Sengerema Mkoani Mwanza.

No comments:

Powered by Blogger.