LIVE STREAM ADS

Header Ads

HALI MBAYA ILIYOPO BUGARIKA JIJINI MWANZA YAMLAZIMU MIRAJI MTATURU KUTOA AGIZO.

Na:George GB Pazzo
Katibu wa Chama cha Mapinduzi CCM Mkoani Mwanza Miraji Mtaturu ametoa muda wa siku nne kwa Halmashauri ya Jiji la Mwanza, kuhakikisha kwamba Uchafu uliozagaa katika dampo la Bugarika Sokoni unaondolewa haraka iwezekanavyo.

Mtaturu alitoa kauli hiyo jumamosi iliyopita alipokuwa akiwahutubia wananchi wa Bugarika Kata ya Pamba Wilayani Nyamagana katika Mkutano wa hadhara ikiwa ni katika kuadhimisha Kilele cha Maadhimisho ya Wiki ya Jumuiya ya Wazazi wa chama hicho Mkoani Mwanza.

“Nimemwelekeza Katibu wa Wilaya (Katibu wa CCM Wilaya ya Nyamagana Elias Mpanda) amwambie Mkurugenzi wa Jiji (Mkurugenzi wa Jiji la Mwanza Halifa Hida) ahakikishe alhamisi sikuti takataka pale, nasema hivyo kwa sababu gani, zile takataka zinazalisha maradhi kwa wananchi”. Alisema Mtaturu.

Aidha alisema kuwa watendaji wa Serikali pamoja na viongozi wa kisiasa wanapaswa kuwatumikia wananchi, na watakaoshindwa kufanya hivyo wanapaswa kuwajibishwa ambapo katika hatua nyingine amewasihi wananchi kutowachagua viongozi wa Kisiasa ambao hawawajibiki katika majukumu yao ambapo amemtolea mfano diwani wa Kata ya Pamba Samwel Range (Chadema) kuwa nae ni miongoni mwa viongozi wasiowajibika kwa ajili ya wananchini.

Mtaturu alibainisha kuwa siku ya alhamisi wiki hii atafika katika damu hilo la Bugarika Sokoni ili kujionea kama uchafu umeondolewa na akikuta bado uchafu huo haujaondolewa basi viongozi wa eneo hilo ambao ni pamoja na Mtendaji wa Kata ya Pamba wajiandae kuwajibika.

Pamoja na kuwasihi wananchi wote kujitokeza kwa wingi kujiandikisha katika daftari la Kudumu la wapiga kura wakati utakapofika, pia aliwahimiza Vijana kuacha kulalamika kuwa hawawezeshwi badala yake wajiunge katika Vikundi ili kuweza kutambulika na hivyo kufikiwa kirahisi kwa ajili ya kunufaika na fursa zinazotolewa na Serikali kwa ajili ya Vijana.
                                 TAZAMA PICHA HAPA

No comments:

Powered by Blogger.