LIVE STREAM ADS

Header Ads

SERIKALI YATAKIWA KUSAIDIA MAPAMBANO DHIDI YA MAAMBUKIZI YA MAGONJWA YA SARATANI.

Washiriki wa Semna ya Uhamasishaji Viongozi wa Afya Mkoani Mwanza kuhusu kupambana na Ugonjwa wa Saratani ya Shingo ya Kizazi wakiwa katika Mafunzo kwa Vitendo mwishoni mwa mwaka jana.
MALONGO MBEHO
Serikali imetakiwa kuendelea kuwawezesha wadau mbalimbali wa afya hapa nchini ili kusaidia katika mapambano dhidi ya maambukizi ya magonjwa ya Saratani.

Hayo yalisemwa jana na Dr.Amina Jumanne Yusuph ambae ni daktari wa magonjwa ya saratani ya shingo ya kizazi kwa akina mama kutoka Hospitali ya Rufaa Bugando wakati akizungumza na Radio Metro Jijini Mwanza.

Dr.Yusuph alisema kuwa bado maambukizi ya Saratani ya Shingo ya Kizazi kwa akina mama hapa nchini yapo juu huku Mikoa ya Kanda ya Ziwa ikiwa katika kiwango kikubwa zaidi cha maambukizi hayo.

Akieleza sababu za Maambukizi hayo kuwa katika kiwango kikubwa hususani katika Mikoa ya Kanda ya Ziwa, Dr.Yusuph alisema kuwa hiyo inatokana na ushiriki wa ngono zembe katika maeneo ya uzalishaji maeneo ya Migodini na Visiwani katika kambi za wavuvi.

Alibainisha kuwa Maambukizi hayo huambukizwa kwa njia ya Kujamiana hivyo maambukizi hayo kwa njia ya zinaa yamekuwa yakiongezeka siku hadi siku hadi kufikia takribani asilimia 99 hapa nchini.

"Serikali iendelea kuwawezesha wahudumu wa afya ili kuendelea kutoa elimu katika jamii kwa lengo la kupambana na Maambukizi ya Saratani ya Shingo ya Kizazi kwa wanawake maana maambukizi haya hugharimu maisha ya wanawake wengi". Alisema Dr.Yusuph na kuongeza;


“Wanajamii pia wanatakiwa kujijengea tabia ya kupima afya zao mara kwa mara kwani Vipimo vya saratani ya shingo ya kizazi hutolewa bila malipo katika hospitali mbalimbali ikiwemo Hospitali ya Rufaa Bugando”.

Inaelezwa kuwa zaidi ya wanawake elfu thelathini na tano kwa mwaka hupoteza maisha hii ikiwa ni kwa kila maambukizi laki moja yanayotokea.
                              SOMA ZAIDI KUHUSU SARATANI HAPA

No comments:

Powered by Blogger.