LIVE STREAM ADS

Header Ads

SERIKALI YAKIRI KUSHINDWA KUFIKIA MALENGO ILIYOJIWEKEA.

ELISA ANATORY
Serikali kupitia Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii imeshindwa kufikia lengo namba tano la maendeleo la milenia katika kuboresha afya ya uzazi kwa mwaka 2015 hivyo inajipanga upya ili kufikia upya malengo hayo hadi kufikia mwaka 2020.

Hayo yalisemwa jana bungeni Mjini Dodoma na naibu waziri wa habari, vijana, utamaduni na michezo Juma Nkamia kwa niaba ya Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Dr.Seif Rashid wakati akijibu swali la mbunge wa viti maalum Anastazia  Wambura aliyetaka kujua mikakati ya serikali juu ya malengo ya milenia kuhusu kuboresha afya ya uzazi nchini.

Waziri Nkamia alisema kuwa lengo namba tano la malengo ya milenia lilikuwa ni kupunguza vifo vya wanawake na watoto vitokanavyo na uzazi kutoka vifo 529 kwa kila vizazi hai laki moja hadi kufikia chini ya vifo 193 kwa vizazi hai laki moja.

“Japokuwa malengo yaliyowekwa hayajafikiwa lakini juhudi za mpango huo zimezaa matunda ambapo takwimu za sensa ya watu na makazi ya mwaka 2012 zinaonyesha kuwa vifo vitokanavyo na uzazi vimeshuka hadi kufikia vifo 432 kwa vizazi hai laki moja”. Alisema Nkamia na kuongeza kuwa Serikali inafanya kila jitihada ili kufikia malengo ya Milenia iliyojiwekea hadi kufikia mwaka 2010.

No comments:

Powered by Blogger.