LIVE STREAM ADS

Header Ads

VIONGOZI CHADEMA WATAKIWA KUWATUMIKIA WANANCHI NA SI KULALAMIKA KILA SIKU.

NA:PRISCA MSHUMBUSI MWANZA.
Katibu wa Jumuiya ya Wazazi wa Chama cha Mapinduzi CCM  Wilaya ya Ilemela Mkoani Mwanza Faisali Dauda, ameutaka uongozi wa chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA kuacha tabia ya kulalamika badala yake kitimize wajibu wake wa kuwatumikia wananchi.

Dauda alitoa kauli hiyo juzi wakati akizungumza nasi ambapo alibainisha kuwa Chama hicho kimekuwa na viongozi ambao kila kukicha wanaishia kuilalamikia CCM kwa kuwa ni chama kilicho madarakani pasipo kuwa na sababu yoyote.

Alieleza kuwa katika nchi hii hakuna hatua yoyote  ya maendeleo iliyochochewa na Chadema, ambapo alitolea mfano barabara mbovu zilizo katika Wilaya ya Ilemela ambayo mbunge wake anatokana na Chadema.

“Barabara ya Nyampara –Kilimahewa  ni mbovu kwani wananchi wanateseka hasa kipindi cha mvua ambapo huwa haipitiki, hivyo nashangaa wanalalamika nini? wakati wao wana diwani na Mbunge. Alisema Dauda.

Aidha alisema kuwa, wao walikabidhiwa madaraka na wananchi ili waweze kutatua matatizo yanayowakabili katika maeneo yao, hivyo kama wameshindwa kutekeleza majukumu ya wananchi wao wakae pembe ili Chama cha Mapinduzi (CCM)  kiendelee kutatua matatzizo ya wananchi wake.


“ Wasiwe kama mfano wa kikojozi, mtu umelala nae usiku akakojoa halafu anakugeuza upande wa mkojo ili uonekane umekojoa wewe, binafsi sikubaliani nao maana daima CCM ndio msingi imara wa kutetea wananchi.” Aliongeza Dauda.

No comments:

Powered by Blogger.