WENYEVITI UKAWA WAGOMEA KIKAO CHA MAENDELEO JIJINI MWANZA NA KUSABABISHA KIKAO KUVUNJIKA.
John Minja (Aliesimama).
Na:Genya Richard
Kikao cha Maendeleo cha Kata ya Igogo Jijini Mwanza Kimeshindwa
Kuendelea baada ya Wenyeviti wa Serikali za Mitaa katika Kata hiyo wanaotokana na Vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi UKAWA kugomea kikao Hicho.
Kikao hicho kilichokuwa
kimeketi jana katika Ofisi ya Kata hiyo ya Igogo, kilivunjika baada ya wenyeviti
wanaotoka katika Vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi Ukawa, kudai
kuwa kilikuwa ni kikao batili na hakina agenda na hivyo kumtaka mwenyekiti
kukiahirisha hadi wakati mwingine kitakapoketi kikiwa na agenda toshelezi.
“…Mwenyekiti unaahirisha
kikao au unataka tufanye vurugu, Maana unatupelekesha unavyotaka wewe…Kwanza
kikao hakina agenda zinazoeleweka…”.Walisikika wakisema wenyeviti wa Mitaa ya
Malulu, Bugando na mingineyo ambao wanatokana na Vyama vya Ukawa huku
wakisimama na kutoka nje ya Ukumbi.
Mwenyekiti wa Kikao hicho John Austino Minja ambae ni Diwani wa Kata ya Igogo (CCM) na Naibu Meya wa Jiji la Mwanza alieleza kusikitishwa kwake kwa hatua ya kikao hicho kuvurugika huku akibainisha kuwa lengo lake lilikuwa ni kujadili mipango ya Maendeleo ya Kata hiyo kwa ajili ya maboresho na kufanikisha kwa wakati ujenzi wa Maabara katika shule za Sekondari Katani hapo.
Mwenyekiti wa Kikao hicho John Austino Minja ambae ni Diwani wa Kata ya Igogo (CCM) na Naibu Meya wa Jiji la Mwanza alieleza kusikitishwa kwake kwa hatua ya kikao hicho kuvurugika huku akibainisha kuwa lengo lake lilikuwa ni kujadili mipango ya Maendeleo ya Kata hiyo kwa ajili ya maboresho na kufanikisha kwa wakati ujenzi wa Maabara katika shule za Sekondari Katani hapo.
No comments: