JB BELMONT HOTEL YA JIJINI MWANZA YAFUNGWA.
Hotel ya nyota tano ya JB Belmont iliyopo
Jijini Mwanza imefungwa kwa kile kilichodaiwa kuwa ni kushindwa kutimiza
masharti ya mkataba kati yake na mmiliki wa jengo ilipo hotel hiyo Mfuko
wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF).
Tangazo la
kufungwa kwa hoteli hiyo lilitolewa juzi jumamosi asubuhi baada ya watumishi wa
NSSF kubadika tangazo la kufungwa huduma katika hotel hiyo jambo lilichosababisha
wateja waliokuwa wakifika hotelini hapo na kushangazwa na tangazo hilo.
Hata hivyo
haikujulikana kama kulikuwa na wateja ndani ya hoteli hiyo kwa kuwa hakuna mtu
aliyeruhusiwa kuingia ndani ya hoteli
hiyo ambapo eneo la mbele ya hoteli hiyo lilizungushiwa kamba kuashiria kwamba
hakuna alieruhusiwa kuingia ndani.
Hoteli hiyo
ambayo inamilikiwa na raia wa Uganda Justus Buguma (marehemu kwa sasa), kabla ya kubadilishwa jina na kuitwa JB
Belmont, ilikuwa ikijulikana kwa jina la Nyumbani Hoteli ikimilikiwa na
aliyewahi kuwa mbunge wa Jimbo la Vunjo
(CCM), Aloyce Kimaro ambaye naye inadaiwa
kuwa aliondolewa na NSSF ndani ya
jengo hilo baada ya kushindwa kulipa kodi.
Taarifa
zaidi zinaeleza kuwa baada ya marehemu
Bugumba kufariki dunia Februari 13, 2013 hoteli hiyo hivi sasa inamilikiwa na
familia yake ambapo tena imekumbana na kisa kile kile kilichomkuta Kimaro.
Akizungumza kwa
njia ya simu, Meneja wa NSSF Kanda ya Ziwa Hamis Fakhi alikiri hoteli hiyo
kufungwa huku akishindwa kubainisha
sababu za kufungwa ambapo aliahidi kuzungumza na waandishi wa habari kesho.
“Ni kweli
tumefunga hoteli hiyo lakini sina amelezo mengine zaidi ya hayo, kwani hata
makubaliano ya mkataba kati ya mmiliki wa hoteli na NSSF yalifanyika makao
makuu,” Amlisema Fakhi.
No comments: